Posts

TANZANIA YAELEZA MAFANIKIO YA UJUMUISHWAJI WATU WENYE ULEMAVU COSP19,YAAHIDI KUIMARISHA UPATIKANAJI TEKNOLOJIA SAIDIZI

Image
Na Mwandishi Wetu, New York, Marekani Serikali ya Tanzania imeeleza mafanikio makubwa iliyoyapata katika kuimarisha ustawi na ujumuishwaji wa watu wenye ulemavu, huku ikisisitiza umuhimu wa kuongeza upatikanaji wa vifaa na teknolojia saidizi ili kuwawezesha kushiriki kikamilifu katika shughuli za kijamii na kiuchumi. Akihitimisha ushiriki wa Tanzania katika Mkutano wa 19 wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Haki za Watu Wenye Ulemavu (COSP19-CRPD) uliofanyika New York, Marekani, Juni 11, 2026, Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, amesema teknolojia na vifaa saidizi vina mchango mkubwa katika kuwawezesha watu wenye ulemavu kuishi kwa kujitegemea na kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya jamii. “Ni muhimu kuendelea kuongeza upatikanaji na matumizi ya vifaa na teknolojia saidizi kwa watu wenye ulemavu ili kuwawezesha kushiriki kikamilifu katika shughuli za kijamii na kiuchumi kwa usawa pia Serikali inaendelea kutekeleza kwa vitendo d...

WAZIRI NDEJEMBI AZINDUA MKOPO WA MAJIKO YA UMEME, VITUO VYA KUCHAJIA MAGARI YA UMEME

Image
-Vituo 50 kujengwa nchini -Wateja milioni moja kunufaika na majiko ya umeme Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, leo Juni 11, 2026 jijini Dodoma amezindua rasmi mpango wa ukopeshaji wa majiko ya umeme kwa wateja wa TANESCO pamoja na mradi wa vituo vya kuchajia vyombo vya usafiri vinavyotumia umeme, hatua inayolenga kuhamasisha matumizi ya nishati safi nchini. Akizungumza katika hafla hiyo, Waziri Ndejembi amesema matukio hayo mawili ni ya kihistoria kwa kuwa yanafungua ukurasa mpya wa matumizi ya umeme nchini, si kwa ajili ya mwanga pekee bali pia kama nyenzo ya kuboresha maisha ya wananchi, kupunguza gharama za maisha na kulinda mazingira. Amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imewekeza kwa kiwango kikubwa katika sekta ya nishati, hali iliyowezesha uzalishaji wa umeme nchini kufikia zaidi ya megawati 4,000 na kuifanya Tanzania kuwa na umeme wa kutosha kwa matumizi mbalimbali ya maendeleo. Kuhusu mpango wa majiko ya umeme, Wazi...

TANZANIA YAONGOZA MJADALA WA KIMATAIFA KUHUSU UIMARISHAJI WA HUDUMA NA UWEZESHWAJI KWA WATU WENYE ULEMAVU

Image
MWISHO Na mwandishi wetu- New York, Marekani. Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Mhe. Balozi Togolani Mavura, ameongoza mjadala wa ngazi ya juu katika Mkutano wa 19 wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Haki za Watu Wenye Ulemavu (COSP19), uliojikita katika mada ndogo ya “Jamii Imara: Kuimarisha Mifumo ya Huduma na Msaada ili Kuhakikisha Uwezeshaji, Uhuru na Kujitegemea kwa Watu Wote Wenye Ulemavu.” Akifungua mjadala huo, Mhe. Balozi Togolani amesema huduma na mifumo ya msaada ni msingi muhimu wa ustawi wa watu binafsi, jamii na uchumi kwa ujumla, huku akisisitiza kuwa utekelezaji wa Mkataba wa Haki za Watu Wenye Ulemavu umeleta mafanikio makubwa duniani katika kipindi cha miaka 20 tangu kupitishwa kwake. "licha ya hatua zilizofikiwa, bado watu wengi wenye ulemavu wanakabiliwa na changamoto za kupata huduma na msaada unaokidhi mahitaji yao, hali iliyodhihirika zaidi wakati wa janga la UVIKO-19 ambapo mifumo mingi ya huduma ilionekana kutokuwa imara na jumuishi vya...

MAHUNDI AIELEZA DUNIA HATUA ZA TANZANIA KATIKA KULINDA HAKI ZA WATU WENYE ULEMAVU

Image
Na Jackline Minja, New York, Marekani Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, ameieleza Jumuiya ya Kimataifa hatua kubwa zinazochukuliwa na Serikali ya Tanzania katika kulinda na kuendeleza haki za watu wenye ulemavu, wakati aliposhiriki Mkutano wa 19 wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Haki za Watu Wenye Ulemavu (COSP19) unaofanyika katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, Jijini New York, Marekani. Mhe. Mahundi, ambaye amemuwakilisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Sera, Bunge na Uratibu  na Wenye Ulemavu, Mhe. Profesa Palamagamba John Kabudi, amesema Tanzania imeendelea kuimarisha mifumo ya kisheria, kisera na kiutendaji ili kuhakikisha watu wenye ulemavu wanapata haki, fursa na huduma stahiki kama wananchi wengine. Akiwasilisha taarifa ya nchi, Mhe. Mahundi amesema Tanzania imepiga hatua kubwa kupitia Sheria ya Watu Wenye Ulemavu Na. 9 ya mwaka 2010 kwa Tanzania Bara pamoja na Sheria Na. 8 ya mwaka 2022 ya Zanz...

UHURU WA VYOMBO VYA HABARI UENDE SAMBAMBA NA UWAJIBIKAJI - KOMANYA

Image
  Na Mwandishi Wetu Weledi, maadili na uelewa wa sheria kwa waandishi wa habari vimetajwa kuwa nyenzo muhimu katika kulinda haki za wananchi na kuhakikisha jamii inapata taarifa sahihi kuhusu masuala ya kisheria, haki za binadamu na ukatili wa kijinsia. Hayo yameelezwa na Mjumbe wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Ladislaus Komanya, tarehe 09 Juni 2026 wakati akiwasilisha mada kuhusu "Uhuru wa Vyombo vya Habari katika Enzi ya Kidijiti: Wajibu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari" katika mafunzo ya waandishi wa habari yaliyoandaliwa na Wizara ya Katiba na Sheria wilayani Tarime, mkoani Mara. Wakili Komanya amesema uhuru wa vyombo vya habari unaenda sambamba na uwajibikaji wa mwandishi katika kuthibitisha taarifa, kuzingatia maadili ya taaluma na kuheshimu sheria za nchi.  Ameongeza kuwa waandishi wa habari wanapaswa kutumia fursa zinazotolewa na teknolojia za kidijiti kwa kuzingatia weledi na maadili ili kuhakikisha taarifa wanazozitoa zinachangia up...

KIPANGULA AWATAKA WAANDISHI KUIPA HADHI TAALUMA YA HABARI

Image
  Na Mwandishi Wetu Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amewashauri Waandishi wa Habari nchini kuipa thamani na heshima taaluma ya habari kwa kuzingatia nadhifu ya mavazi na mienendo yao wanapotekeleza majukumu ya kitaaluma. Wakili Kipangula ametoa ushauri huo leo Juni 5, 2026 wakati akiwasilisha mada kuhusu “Uhuru wa Vyombo vya Habari katika Enzi ya Kidijiti: Wajibu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari” kwenye Kongamano la Uhuru wa Vyombo vya Habari lililoandaliwa na Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) kupitia Idara ya Sanaa na Taaluma za Habari. Amesema uandishi wa habari ni taaluma muhimu inayotambulika kama muhimili wa nne usio rasmi katika jamii, hivyo ni wajibu wa waandishi wenyewe kuhakikisha wanaijengea heshima kupitia mwenendo, maadili na namna wanavyojiwasilisha mbele ya jamii. Wakili Kipangula amesema mwonekano wa mwandishi wa habari unaweza kuwa sehemu ya kujenga imani kwa jamii na vyanzo vya habari vinavyotoa...