WIZARA YA MADINI YAKUTANA NA UJUMBE WA WAWEKEZAJI KUTOKA CHINA KUJADILI FURSA ZA USHIRIKIANO SEKTA YA MADINI
📍 Dodoma Wizara ya Madini imekutana na ujumbe wa wawekezaji kutoka Jamhuri ya Watu wa China unaotoka katika Kampuni ya Kimataifa ya Liaoning Fangda Group, kwa lengo la kujadili na kubaini maeneo ya kimkakati ya ushirikiano katika kuendeleza Sekta ya Madini nchini Tanzania. Ujumbe huo uliongozwa na Makamu Mwenyekiti wa Kampuni hiyo, Bw. Ao Xinhua, ambaye ameambatana na wataalamu mbalimbali kutoka Sekta za Viwanda, Madini na Teknolojia. Kikao hicho kilifanyika Machi 30, 2026 katika Ukumbi wa Tume ya Madini jijini Dodoma, kikiongozwa na Kamishna wa Madini, Dkt. AbdulRahman Mwanga. Katika majadiliano hayo, pande zote mbili zilijikita katika kuchambua fursa mbalimbali zilizopo katika mnyororo mzima wa thamani wa Sekta ya Madini, ikiwemo utafiti wa madini, uchimbaji, uongezaji thamani (beneficiation), pamoja na uwekezaji katika teknolojia za kisasa za uchakataji wa madini. Akizungumza wakati wa kikao hicho, Dkt. Mwanga alieleza kuwa Tanzania ina mazingira rafiki ya uwekezaji, sera thabiti n...