Posts

Showing posts from April, 2025

DKT. BITEKO AWATAKA TPDC KUONGEZA KASI UENDELEZAJI VITALU VYA MAFUTA,GESI ASILIA

Image
Naibu  Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko ameliagiza Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC)  kuongeza kasi ya uendelezaji wa Vitalu vya utafutaji wa Mafuta na Gesi Asilia ikiwemo Mnazi Bay Kaskazini, Eyasi Wembere, Songo Songo Magharibi na Mradi wa Kuchakata na Kusindika Gesi Asilia (LNG) ili nchi iendelee kuwa na uhakika wa upatikanaji wa nishati kwa ajili ya soko la ndani na nje. Ameyasema hayo leo jijini Dodoma wakati akizindua Mkakati wa Muda Mrefu wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) wa miaka 25 (2024/25 hadi 2049/50) ambao umeweka mipango na malengo makubwa ya kuleta uhakika wa upatikanaji wa nishati nchini, mkakati ambao utaisaidia nchi kutumia kikamilifu rasilimali za mafuta na gesi zilizopo katika maeneo mbalimbali.  ”Tunapozindua Mpango Mkakati huu wa miaka 25, ni muhimu tutambue kuwa  jukumu muhimu la TPDC ni kuhakikisha kunakuwa na upatikanaji wa nishati nchini. Ni muhimu sisi sote hapa tukumbuke kuwa Sekta ndogo ya ...

JKI YAWAFUNDA WANAWAKE KUEPUKA MIKOPO KANDAMIZI 'KAUSHA DAMU'

Image
Taasisi isiyo ya kiserikali ya Jamii Kwanza Initiative(JKI) kwa Kushirikiana na Ofisi ya Serikali ya Mtaa wa Amani Leo April 29,2025 imetoa mafunzo kwa wanawake kuhusu athari ya mikopo kandamizi (kausha damu) ili kuwawezesha kuepukana na adha na udhalilishaji wanaoupata wanapodaiwa. Akizungumza wakati akifungua mafunzo hayo ambayo yamefanyika kata ya Kipunguni,Wilaya ya Ilala Jijini Dar es salaam Mkurugenzi wa (JkI) Daniel Joseph Migera amesema kuwa wameamua kutoa mafunzo hayo ili kuwasaidia wanawake kujikwamua kiuchumi. "Wanawake wanapata changamoto na shida ambazo zinawafanya wakachukue mkopo ili waweze kuzitatua lakini badala ya wanaangukia kwenye mikopo ambayo inakuwa si yenye faida kwao" Amesema Migera. Amesema kuwa Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan imeweka mipango ya kuwasaidia wanawake kujikwamua kiuchumi kwa kuwapatia mikopo ya asilimia kumi ,hivyo kwa mafunzo wanayoyatoa watapata Elimu ya Fedha ambayo itawasaidia kwenye biashara zao.   Kwa upande wake Katibu wa Ch...

EKARI 41 ZATENGWA KWA AJILI YA OFISI ZA TANAPA ENEO LA KANZUNGU BUNDA

Image
Na. Anangisye Mwateba-Bungeni Dodoma Wizara ya Maliasili na utalii, kupitia shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) imetenga eneo lenye ukubwa wa ekari 41.13 katika eneo la Kunzugu, Kata ya Balili, Mjini Bunda kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi za TANAPA Kanda ya Magharibi. Haya yamebainishwa na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dunstan Kitandula(Mb) alipokuwa akijibu swali la Mhe. Robert Chacha Maboto aliyetaka kujua Serikali itajenga lini Makao Makuu ya TANAPA katika Halmashauri ya Mji wa Bunda. Aidha Mhe. Kitandula aliongeza kuwa Serikali imekamilisha zoezi la upembuzi yakinifu na uandaaji wa michoro kwa ajili ya ujenzi wa ofisi hiyo. Kazi ya ujenzi inatarajiwa kuanza kwenye mwaka wa fedha 2025/2026.

TIJA KWA NCHI NDIYO KIPAUMBELE CHA UTEKELEZAJI WA MRADI WA KUCHAKATA NA KUSINDIKA GESI ASILIA (LNG)- DKT.BITEKO*

Image
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt.Doto Biteko amesema dhamira ya Serikali ni kutekeleza mradi mkubwa wa Kuchakata na Kusindika Gesi Asilia (LNG) kutokana na faida zake kiuchumi ila kwa sasa kuna maeneo ambayo Serikali inayafanyia kazi kwa kina kupitia majadiliano na Wawekezaji ili mradi husika uwe na tija kwa nchi na wananchi. Ameyasema hayo tarehe 29 Aprili 2025 bungeni jijini Dodoma wakati akijibu hoja mbalimbali zilizotolewa na Wabunge kuhusu Hotuba ya Bajeti ya  Wizara ya Nishati ya shilingi Trilioni 2.2 kwa mwaka 2025/2026 kabla ya kupitishwa kwa kishindo na Bunge hilo kwa asilimia 100. “ Mradi wa LNG umeanza kusemwa kwa muda mrefu na kila mmoja angetamani mradi huu ukamilike jana lakini lazima tukubaliane kuwa lazima tujadiliane kwa kina na wawekezaji ili kupata kilicho bora na kuleta tija, ninachotaka kuwahakikishia ni kuwa timu ya majadiliano ya Serikali na Wawekezaji wanaendelea na majadiliano na tunatarajia kuwa ndani ya mwaka huu 2025 kama tutakuwa tumemal...

WATENDAJI UBORESHAJI WA DAFTARI AWAMU YA PILI WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA

Image
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akizungumza na watendaji wa uboreshaji ngazi ya Kata na Waandishi Wasaidizi na Waendesha vifaa vya Biometriki kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Iringa mkoani Iringa leo Aprili 29,2025 wakati alipotembelea mafunzo hayo ikiwa ni maandalizi ya awamu ya pili mzunguko wa kwanza wa uboreshaji Daftari la Kudumu la Wapiga Kura unaoanza Mei Mosi hadi Mei 07, 2025 katika mikoa 15. Sehemu ya Washiriki wa Mafunzo hayo wakimsikiliza Mwenyekiti wa Tume. Sehemu ya Washiriki wa Mafunzo hayo wakimsikiliza Mwenyekiti wa Tume. Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akikagua mafunzo ya watendaji wa Uboreshaji ngazi ya Kata kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Iringa leo Aprili 29,2025 ikiwa ni maandalizi kuelekea awamu ya pili ya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na uwekaji wazi wa Daftari la awali la wapiga Kura.  Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe....

RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI WA VIONGOZI MBALIMBALI

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amefanya Uteuzi wa Viongozi mbalimbali  kama ifuatavyo;

SERIKALI ITAFANYIA KAZI HARAKA MAAZIMIO YA KONGAMANO LA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI

Image
Wadau na Waandishi wa Habari wakifuatilia uwasilishaji wa mada na majadiliano katika siku ya kwanza ya Kongamano la Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari lililofanyika leo tarehe 28 Aprili, 2025 jijini Arusha. Na Mwandishi Wetu. Serikali imesema itahakikisha inafanyia kazi mapendekezo yote yatakayotolewa kwenye maazimio ya pamoja ya Waandishi wa Habari baada ya kuhitimisha Kongamano la Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari kwa mwaka 2025. Hakikisho hilo la Serikali limetolewa leo tarehe 28 Aprili, 2025 na Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Bw. Gerson wakati akitoa neno la kufunga Siku ya Kwanza ya Kongamano hilo linalofanyika jijini Arusha kwa uratibu wa Jamii Africa, UNESCO na Wizara yenyewe. "Nimesikia maazimio ya awali mliyoyatoa hapa, ni muhimu sana na mimi nitaomba mkishakamilisha ile nakala ya mwisho mtupatie ili na sisi serikalini yale ambayo tunatakiwa tuchukue hatua tuyafanyie kazi, basi tutafanyia...