Posts

Showing posts from May, 2026

WAPIGA KURA 222,218 KUPIGA KURA JIMBO LA ISMANI NA KATA 12 TANZANIA BARA

Image
NA MWANDISHI WETU, IRINGA WAPIGA Kura 222,218 walioandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura watashiriki kwenye uchaguzi mdogo wa Ubunge katika Jimbo la Isimani lililopo Halamashauri ya Wilaya ya Iringa Mkoani Iringa na Kata 12 za Tanzania Bara.   Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele ameyasema hayo leo Mei 31, 2026 Mkoani Iringa wakati akisoma risala maalum kuhusu uchaguzi katika jimbo na kata husika utakao fanyika kesho Juni 01, 2026 na kusema kuwa jumla ya vituo 628 vya Kupigia Kura vitatumika.   “wapiga kura 89,753 wapo kwenye Jimbo la Ismani na wapiga kura 132,465 wapo kwenye kata 12 zitakazofanya uchaguzi mdogo na vituo 277 vipo kwenye Jimbo la Ismani na vituo 351 vipo kwenye kata 12 zitakazofanya uchaguzi mdogo.,”amesema Jaji Mwambegele.   Aidha, amesema Katika Uchaguzi huu, jumla ya wagombea 108 kutoka katika vyama vya siasa 17 wanawania nafasi wazi ya ubunge na udiwani katika maeneo niliyoyataja. “Jimbo la Ism...

JK AKUTANA TENA NA CATHERINE, MIAKA 18 BAADA YA UPASUAJI WA MOYO

Image
Rais mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, leo Mei 29, 2026 amekutana tena na Bi. Catherine P. Conrad Minja, aliyefanyiwa upasuaji wa moyo kwa mafanikio akiwa na umri wa miaka minne katika taasisi ya  Muhimbili Orthopaedic Institute  (MOI) miaka 18 iliyopita. Wakati huo madaktari bingwa wa Moyo wa Taasisi ya Moyo ya JKCI walikuwa wakitumia majengo ya MOI kabla jengo lao halijakamilika. Mara ya kwanza wawili hao walikutana Novemba 14, 2008 wakati Dkt. Kikwete akiwa Rais alipokwenda kumjulia hali Catherine  hapo MOI baada ya kufanyiwa upasuaji wa moyo mapema wiki hiyo. Wakati huo Catherine alikuwa mmoja wa wagonjwa wa mwanzo kufanyiwa upasuaji huo katika taasisi hiyo. Miaka 18 baadaye, Catherine amekua na sasa ni mwanafunzi wa mwaka wa kwanza wa Shahada ya Udaktari katika Chuo Kikuu cha Kairuki  jijini Dar es salaam. Alifika ofisini kwa Rais Mstaafu kumsabahi na kumshukuru kwa mchango wake katika kuanzisha na kuimarisha huduma za matibabu ya magonjwa ya m...

JAJI MWAMBEGELE AWAPA NENO MAKARANI WA UCHAGUZI ISIMANI

Image
  Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Mahakama ya Rufaa    Mhe.Jacobs Mwambegele akizungumza wakati alipotembelea mafunzo ya siku moja kwa Makarani  waogozaji Wapiga Kura katika Jimbo la Isimani yaliyofanyika katika Shule Sekondari Ufundi Ifunda mkoani Iringa ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Uchaguzi huo utakaofanyika Jumatatu ya Juni 1, 2026. Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Mahakama ya Rufaa    Mhe.Jacobs Mwambegele akizungumza wakati alipotembelea mafunzo ya siku moja kwa Makarani  waogozaji Wapiga Kura katika Jimbo la Isimani yaliyofanyika katika Shule Sekondari Ufundi Ifunda mkoani Iringa ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Uchaguzi huo utakaofanyika Jumatatu ya Juni 1, 2026. Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Mahakama ya Rufaa    Mhe.Jacobs Mwambegele amewataka watendaji wa uchaguzi ambao ni Makarani waongozaji Wapiga kura kufanya kazi yao kwa kufuata Sheria, Kanuni na ...

TANZANIA YAJIPANGA KUWA MZALISHAJI MKUBWA WA MADINI KINYWE (GRAPHITE) DUNIANI

Image
Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde  amesema kwamba Tanzania inajipanga kuwa mmoja ya wazalishaji wakubwa Duniani wa madini kinywe(𝙂𝙧𝙖𝙥𝙝𝙞𝙩𝙚) kupitia Kampuni 30 zinazomiliki Leseni za kati na kubwa za uchimbaji wa madini hayo na hivyo kutoa ushindani wa kiuzalishaji kwa nchi ya China ambayo ndio inaongoza kwa uzalishaji wa madini hayo duniani kwa kuzalisha tani milioni 1.2 kwa mwaka.  Mhe Mavunde ameyasema hayo leo  Mei 28,  2026 Wilayani Ruangwa, Lindi aliposhiriki katika hafla ya utiaji saini wa mikataba wa ubia baina ya Serikali na Kampuni ya Lindi Jumbo Limited kwa ajili ya mradi mkubwa wa uchimbaji madini kinywe na kubainisha kuwa kuanza kwa uchimbaji mkubwa wa madini mkakati ya kinywe (graphite) kunaiweka Tanzania kwenye dira ya duniani kama Nchi ya kimkakati katika uzalishaji wa madini hayo muhimu kwenye utengenezaji wa betri za magari ya umeme. "Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameendelea kuijenga na kuifanya nchi yetu ya Tanzania kama Taifa lenye...

TMA,EMEDO KUTOA TUZO KWA WANAHABARI WANAOELIMISHA JAMII TAHADHARI ZITOKANAZO NA HALI YA HEWA

Image
DAR ES SALAAM Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania(TMA) kushirikiana na Shirika la Usimamizi wa Mazingira na Maendeleo (EMEDO) limeungana kuanzisha kutoa tuzo za waandishi wa habari wanaoelimisha jamii kuhusiana na changamoto, matukio ya hali mbaya ya hewa na tahadhari zitokana na usalama kwenye maji. Afisa Uchechemuzi kutoka Shiriki la Usimamizi wa Mazingira na maendeleo(EMEDO) Mary Francis Mahemba amesema, wametambua mchango unaofanywa na vyombo vya habari kuwa ni muhimili muhimu katika kuifikia jamii kutoa taarifa sahihi zitakazoweza kuokoa maisha, kupunguza athari za majanga yanayohusianana hali ya hewa pamoja na kuimarisha uelewa wa jamii kuhusu usalama wa majini. Amefafanua tuzo hizo zinalenga kuhasamasisha utayarishaji wa habari zenye ubora kuhusu matukio ya hali mbaya ya hewa na athari zake kwa jamii, tahadhari za mapema za hali ya hewa, usalama wa vyombo vya usafiri na usafirishaji kwenye maji, uzuiaji wa ajali na vifo vitokanavyo na kuzama maji, pamoja na ustahimilivu wa jamii dh...

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO

Image

HAJI MANARA ATEULIWA KUWA MSEMAJI WA TIMU ZOTE ZA TAIFA

Image
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amemteua Haji Manara kuwa msemaji wa timu zote za Taifa za Tanzania zinazoshiriki mpira wa miguu. Makonda ametangaza uteuzi huo leo Mei 28, 2026 wakati akizungumza na waandishi wa habari katika Viwanja vya Bunge jijini Dodoma. Kwa mujibu wa Waziri huyo, Haji Manara atafanya kazi chini ya Baraza la Michezo la Taifa (BMT) ambapo jukumu lake kubwa litakuwa kuzungumzia na kuratibu mawasiliano ya timu zote za Taifa upande wa mpira wa miguu. Makonda amesema uteuzi huo ni sehemu ya jitihada za kuongeza nguvu katika mawasiliano, masoko pamoja na taswira ya timu za Taifa ndani na nje ya nchi. Haji Manara ni mmoja wa watu maarufu katika masuala ya mawasiliano ya michezo nchini Tanzania, akiwa amewahi kufanya kazi na klabu mbalimbali kubwa za soka nchini. Uteuzi huo umeanza kuzua mjadala mkubwa miongoni mwa mashabiki wa soka na wadau wa michezo nchini huku wengi wakisubiri kuona mchango wake katika kuimarisha mawasiliano ya timu za Taifa...

TARURA YAPATA DOLA MILIONI 65 KUTEKELEZA MIRADI YA DHARURA

Image
Serikali imeiwezesha Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) kupata dola milioni 65 kwa ajili ya utekelezaji wa matengenezo ya miundombinu ya barabara kupitia mfuko wa dharura (CERC). Hayo yamesemwa na Mtendaji Mkuu wa TARURA, Mhandisi Victor Seff wakati wa ziara ya wajumbe wa Bodi ya Ushauri ya Wakala huo katika mradi wa ujenzi wa daraja lenye urefu wa Mita 22 pamoja na barabara za maingilio zenye urefu wa Mita 290 kwenye  barabara ya Ndovelwa yenye urefu wa Km. 20.2 katika Manispaa ya Tabora. Mhandisi Seff amesema fedha hizo ni mkopo nafuu kutoka Benki ya Dunia uliotolewa kufuatia tathmini ya uharibifu wa miundombinu uliosababishwa na mvua za El-Nino za mwaka 2024. Amesema  tathmini hiyo ilibaini maeneo mengi ya barabara yaliyoharibiwa na hivyo kuhitaji matengenezo ya haraka ili kurejesha mawasiliano na huduma kwa wananchi. “Miradi hii inatekelezwa nchi nzima na kwa wastani utekelezaji wake umefikia asilimia 70. Kazi zote zinatarajiwa kukamilika ifikapo Septemba 20...

TANESCO YATAMBULIWA KAMA SEKTA WEZESHI NA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM (UDSM)

Image
Na Mwandishi Wetu Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limetambuliwa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kama miongoni mwa sekta wezeshi zinazochangia maendeleo ya elimu jumuishi na ustawi wa wanafunzi chuoni hapo. Utambuzi huo umetolewa Mei 26, 2026, wakati wa hafla maalum ya kuwatambua na kuwapongeza wadau wa maendeleo wa chuo hicho iliyofanyika katika Ukumbi wa Maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Mhe.Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete, amesema mchango wa wadau mbalimbali wakiwemo TANESCO una mchango mkubwa katika kuboresha mazingira ya kujifunzia na maendeleo ya kitaaluma kwa wanafunzi. “Tunapowasaidia wanafunzi hawa, hatuwafanyii fadhila. Tunathibitisha uwezo wao, utu wao na nafasi yao halali katika elimu ya juu,” amesema Dkt. Kikwete. Aidha, ameshukuru wadau wote wa maendeleo kwa kuendelea kushirikiana na chuo hicho katika kuhakikisha upatikanaji wa elimu jumuishi kwa wanafunzi wote,...

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO

Image
 

RAIS SAMIA MGENI RASMI HAFLA YA KUHITIMISHA MAFUNZO YA MAAFISA NA WAKAGUZI WASAIDIZI 719

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa Mgeni Rasmi katika Sherehe ya Kufunga Mafunzo ya Maafisa na Wakaguzi Wasaidizi wa Jeshi la Polisi ambayo yamechukua miezi sita ambapo kesho tarehe 28/5/2026 mafunzo hayo yakihitimishwa ambapo wahitimu Mia Saba na Kumi na Tisa wakitarajiwa kuhitimu mafunzo hayo. Akizungumza baada ya kutembelea na kukagua maandalizi ya shughuli hiyo na maeneo ya Chuo cha Taaluma ya Polisi, jijini Dar es Salaam ambapo mafunzo hayo yamefanyika, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Patrobas Katambi amesema ni maboresho makubwa yamefanywa katika Jeshi la Polisi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ,Dkt.Samia Suluhu akigusia na maeneo mengine yaliyofanyiwa maboresho makubwa.

MTWARA YATANUA FURSA ZA MADINI, MAPATO YA SERIKALI YAPANDA MARA NNE

Image
Mkoa wa Mtwara umeendelea kujidhihirisha kama kitovu muhimu cha uwekezaji wa madini nchini kutokana na uwepo wa rasilimali nyingi za madini ya viwandani, vito na madini mkakati, huku mapato ya Serikali kupitia sekta hiyo yakiongezeka kwa kasi katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita. Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Mtwara, Winnifrida Mrema, amesema mkoa huo unafahamika zaidi kwa uwepo wa madini ya chokaa yanayotumika kuzalisha saruji katika Kiwanda cha Saruji cha Dangote, jambo linalochangia kukuza uchumi wa mkoa na kuimarisha shughuli za viwanda nchini. Amesema Mkoa wa Mtwara pia una utajiri wa madini mengine ya viwandani yakiwemo chuma, shaba, kinywe, ulanga pamoja na madini ya mchanga mzito (heavy mineral sands), ambayo ni miongoni mwa madini mkakati yanayohitajika kwa kiwango kikubwa duniani katika utengenezaji wa teknolojia mbalimbali ikiwemo magari ya umeme. Aidha, amesema Bandari ya Mtwara imeendelea kuwa kiungo muhimu cha biashara na usafirishaji wa madini na bidhaa za viwandani...

USALAMA WAIMARISHWA SIKUKUU YA EID AL-ADHA

Image
 

WANAHABARI WATAKIWA KUTAFAKARI UPYA WAJIBU WAO KWA JAMII

Image
 Mwenyekiti wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Bw. Tido Mhando, amewataka Waandishi wa Habari nchini kutafakari upya wajibu wao katika kuijenga jamii kupitia maudhui yenye tija, akieleza kuwa ipo haja ya kurejesha hadhi na nguvu ya taaluma hiyo katika kujenga fikra na maendeleo ya taifa. Akizungumza jijini Dar es Salaam, Bw. Mhando amesema pamoja na JAB kusimamia utoaji wa ithibati kwa kuzingatia vigezo vya elimu na sheria, bado kuna umuhimu wa Waandishi wa Habari kuendelea kujengewa uwezo kupitia mafunzo ya kitaaluma. “Tukitazama baadhi ya vyombo vyetu vya habari, iwe ni magazeti, redio au televisheni, mambo ya kufikirisha kwa kiasi kikubwa yamepungua. Waandishi wa Habari wanapaswa kutafakari kama hiyo ndiyo taswira wanayotaka kuiacha katika jamii ya Watanzania,” amesema. Amesisitiza kuwa vyombo vya habari vina nafasi kubwa ya kuunda mtazamo wa jamii, hivyo kuna wajibu wa kuhakikisha maudhui yanayotolewa yanajenga uelewa, yanakuza maendeleo na yanalinda maslahi ya t...

SERIKALI YAENDELEA KUTENGA MAENEO MAPYA KWA WACHIMBAJI WADOGO,LESENI 108 ZATOLEWA

Image
📍Dodoma Serikali imeendelea kuimarisha mazingira ya uwekezaji na ushiriki wa wananchi katika Madini kwa kuendelea kutenga maeneo maalum kwa ajili ya wachimbaji wadogo nchini, hatua inayolenga kuongeza fursa za ajira, kuinua uchumi wa wananchi na kurasimisha shughuli za uchimbaji mdogo.  Katika utekelezaji wa hatua hiyo, Serikali tayari imetenga eneo la Nyakafulu, Wilaya ya Mbogwe Mkoani Geita kwa wachimbaji wadogo na kutoa leseni 108 baada ya kufutwa kwa leseni zilizokuwa haziendelezwi ipasavyo. Hatua hiyo imebainishwa bungeni leo Mei 26, 2026 na Naibu Waziri wa Madini, Mhe. Dkt. Steven Kiruswa kwa niaba ya Waziri wa Madini wakati akijibu maswali ya wabunge kuhusu maendeleo ya Sekta ya Madini. Akijibu swali la Mbunge wa Mbogwe, Mhe. Fagason Nkingwa aliuliza kuwa ni lini Serikali itatenga maeneo kwa wachimbaji wadogo na kuwapatia leseni za uchimbaji, Dkt. Kiruswa amesema Serikali tayari imetenga eneo la Nyakafulu kwa ajili ya wachimbaji wadogo na kutoa jumla ya leseni 108 baada ya ...