Posts

Showing posts from February, 2025

DKT.KAZUNGU AFANYA MAZUNGUMZO NA TAASISI YA AEE INTEC YA AUSTRIA

Image
  Naibu katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Dkt. Khatibu Kazungu amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Teknolojia Endelevu ya Nishati (AEE INTEC) ya nchini Austria, Bw. Christopher Brunner ambaye ameeleza nia ya  kampuni hiyo kuwekeza katika teknolojia mpya ya Joto la Jua (Solar thermal) inayotumika katka kuchemsha maji yanayoweza kutumika katika Shule, Hospitali, Vyuo, Viwanda na Masoko ambayo inawezesha  kupunguza matumizi ya umeme. Mazungumzo hayo yamefanyika jijini Gaborone nchini Botswana ambapo Dkt Kazungu anaongoza  Ujumbe wa Tanzania kushiriki Wiki ya Nishati Endelevu kwa Nchi za Jumuiya ya Kusini mwa Afrika (SADC). “Tanzania tuna rasilimali ya kutosha ya Jua ambayo inaweza kutumika kwa shughuli mbalimbali za kijamii na kiuchumi. tunahitaji teknolojia rahisi  za kisasa na za gharama nafuu katika kuendeleza nishati ya Jua.” Amesema Kazungu Katika kuhakikisha Tanzania inanufaika na programu hiyo kupitia Jumuiya ya Nchi za Kusini m...

WAZIRI KABUDI KUZINDUA BODI YA ITHIBATI YA WAANDISHI WA HABARI MACHI 3.

Image
  Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Palamagamba Kabudi, Wiki ijayo anatarajiwa kuzindua Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB). Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali, Bw. Gerson Msigwa imeeleza kuwa uzinduzi huo unatarajiwa kufanyika tarehe 03 Machi, 2025 katika Hotel ya Johari Rotana jijini Dar es Salaam. Katika Uzinduzi huo Waziri Kabudi pia atamkabidhi zana za Kazi Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Bw. Tido Mhando, zinazojumuisha Sera ya Habari, Sheria ya Huduma za Habari na Kanuni zake. Miongoni mwa majukumu ya Bodi hiyo yanayotarajiwa kuanza kutekelezwa mapema mara baada ya kuzinduliwa ni pamoja na kutoa Ithibati na Vitambulisho (Press Card) kwa Waandishi wa Habari waliokidhi vigezo vilivyoainishwa kisheria na kusimamia maadili ya taaluma ya Uandishi wa Habari. Kwa kuzingatia matakwa ya Sheria ya Huduma za Habari, Sura ya 229, Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari imepewa mamlaka ya kutoa Vitambulisho kwa Wa...

SERIKALI IMEONDOA CHANGAMOTO WALIZOKUTANA NAZO WANAWAKE KATIKA UONGOZI - BI. BAHATI MTONO

Image
Mkurugenzi Msaidizi Sehenu ya Usimamizi wa Rasilimaliwatu Wizara ya Nishati, Bi. Bahati Mtono amesems Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imeondoa  changamoto waizokutana nazo wanawake katika umiliki wa ardhi na masuala ya uongozi. Bahati ameyasema hayo alipokuwa akielezea historia ya mwanamke katika kutetea haki zake katika kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake  Duniani.  "Historia inaonesha miaka ya 1910 kulikuwa na harakati mbalimbali ambapo wanawake walijipanga kupigania haki zao na mwaka 1975  Umoja wa Mataifa ulianzisha siku ya Wanawake Duniani." Amesema Bi. Mtono Ameeleza kuwa, lengo hasa la kuanzisha siku hiyo ni kupambania haki za mwanamke na kuikumbusha Dunia kuhakikisha inazingatia wanawake katika  upatikanaji wa haki za msingi lakini pia masuala ya usawa wa  kijinsia kati ya wanawake kuhakikisha wote wanapata haki zao za msingi. Amesema Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Nishati zinajitahidi kusaidia wanawake akitolea mfano Shirika la...

SERIKALI YAVUNA SHILINGI BILIONI 183 MASOKO YA MADINI

Image
•Ni mwaka wa fedha 2023/2024 •Masoko ya madini yafikia 43, vituo 109 •Wanolewa matumizi sahihi ya XRF Wakati masoko ya madini yakifikia 43, mchango wa masoko hayo umeongezeka kutoka Shilingi Bilioni 8 mwaka 2018/ 2019 hadi Shilingi Bilioni 183 mwaka wa fedha uliomalizika wa 2023/2024. Akizungumza katika mafunzo ya  matumizi ya mashine maalum ya kupima madini ya metali kwa njia ya MIONZI /X-RAY,  kwa maafisa masoko wa madini Mkurugenzi wa Ukaguzi na Biashara ya Madini, Venance Kasiki amesema mbali na masoko hayo pia kuna vituo vya ununuzi wa madini 109. Amesema, “Kwa kuzingatia asilimia kubwa ya mapato yetu katika masoko yanatokana na madini ya dhahabu, na ili tupate maduhuli lazima tutumie  mashine za XRF kupima asilimia (purity) ya madini yanayouzwa. Majibu yanayotokana na XRF yanatumika  kukokotoa mrabaha  na ada ya ukaguzi,”. Kwa upande wa Meneja wa Biashara ya Madini Sundi Malomo akizungumza amesema kuwa tangu Serikali kupitia Tume ya Madini  kuanzisha ...

SERIKALI KUENDELEA KUTUNGA SERA RAFIKI KUWEZESHA USHIRIKI WA SEKTA BINAFSI KATIKA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

Image
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema Serikali itaendelea kutunga Sera rafiki zitakazowezesha ushiriki wa sekta binafsi katika upatikanaji wa nishati safi ya kupikia kwa bei nafuu. Ameyasema hayo leo Februari 27, 2025 akiwa wilayani Muheza katika muendelezo wa ziara yake mkoani Tanga ambapo amezindua zoezi la ugawaji wa mitungi ya gesi ya kupikia kwa wananchi wa Mkoa wa Tanga. "Tumeanza kutoa ruzuku kwa wale wote wenye miradi ya gesi ambao wanachakata na kuifanya gesi kuwa nishati". Amesema Rais Samia Ameongeza kuwa,  Serikali pia inatoa ruzuku hadi kwenye majiko ya umeme ili kuwezesha watanzania wengi zaidi kutumia nishati safi ya kupikia.  Amepongeza ubunifu wa teknolojia mbalimbali  ambazo zinakwenda kubana matumizi katika kutumia nishati safi ya kupikia. Amesema  lengo la Serikali ni kulinda afya za watumiaji wa Nishati za kupikia pamoja na mazingira. Aidha, Rais Samia ameitaka Wizara ya Nishati kuendelea kuusimamia...

WANAWAKE TUNAPOPATA FURSA TUSIMAME NA TUTENDE HAKI - MKURUGENZI UNUNUZI NISHATI

Image
Mkurugenzi wa Ununuzi Wizara ya Nishati,  Bi. Marieta Kiago ametoa rai kwa Wanawake hususan vijana kuwa wanapopata nafasi za kufanyakazi kwenye maeneo na Taasisi mbalimbali kuhakikisha wanasimama imara na kuitenda haki kwa wananchi. Bi. Kiaho ameyasema hayo alipokuwa akielezea nafasi ya Msichana katika kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambayo nchini yatafanyika mkoani Arusha. "Ninachotaka kusema katika kuelekea maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani wale tunaopata nafasi basi  tuzitendee haki hasa tunapotoa huduma kwa wananchi."  Amesema Bi. Kiago Amesema miaka ya nyuma hakukuwa na haki kwa wanawake katika masuala mbalimbali tofauti na sasa ambapo haki za mwanamke zinazidi kutambuliwa na kuheshimiwa. Akizungumzia  kuhusu usawa Bi. Kiago amesema  unatakiwa kuwepo katika jinsia zote kwa wanawake na wanaume ambapo ameipongeza Serikali kwa kuweka usawa katika utekelezaji wa majukumu kwenye jamii.  Ameongeza kuwa kwa sasa wanawake wengi wameshika...

INEC YATANGAZA KUANZA MCHAKATO WA KUGAWA MAJIMBO YA UCHAGUZI

Image
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imetangaza kuanza kwa mchakato wa kuchunguza na kugawa au kubadili majina ya majimbo ya uchaguzi ambapo itapokea mapendekezo kuanzia tarehe 27 Februari, 2025 hadi tarehe 26 Machi, 2025. Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Rufani, Jacobs Mwambegele leo tarehe 26 Februari, 2025 muda mfupi baada ya kumaliza kuongoza kikao cha Tume kilichofanyika mkoani Morogoro.  " Kwa kuzingatia masharti ya Kanuni ya 18(1) ya Kanuni za Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi za mwaka 2024, napenda kutoa taarifa kwa umma kwamba, kuanzia kesho siku ya Alhamis tarehe 27 Februari, 2025 Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi itaanza mchakato wa kuchunguza na kugawa au kubadili majina ya majimbo ya uchaguzi,"   amesema Jaji Mwambegele. Akifafaunua kuhusu muda wa kupokea maombi, Jaji Mwambegele amesema maombi yote ya kugawa au kubadilisha jina la jimbo yawasilishwe Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi kuanzia tarehe 27 Februari, 2025 hadi tarehe 26 Ma...

DKT. BITEKO AHIMIZA MSHIKAMANO, UPENDO NA UMOJA MSALALA

Image
-Awaasa Wanamsalala kuchagua maendeleo badala ya maneno -Rais Samia atakeleza Ilani ya CCM kwa 99% Msalala Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa angependa kuona wananchi wa Kahama wanashirikiana na kuungana kwa pamoja katika shughuli za maendeleo ya Wilaya yao. Aidha, amewaasa kutoacha msingi wa Chama Cha Mapinduzi wa kuwaletea wananchi maendeleo na kwamba Taifa linategemea CCM iwahudumie na sio kuruhusu mipasuko miongoni mwao. Dkt. Biteko ameyasema hayo Februari 25, 2025 Kahama, mkoani Shinyanga wakati aliposhiriki katika Mkutano Maalum wa Chama Cha Mapinduzi Jimbo la Msalala uliolenga kuwasilisha Taarifa ya Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM mwaka 2020-2025. Akizungumzia fursa za maendeleo zilizopo wilayani humo, Dkt. Biteko amesema  kuwa Kahama ni Wilaya  ya kimkakati ambayo ina bandari kavu iliyopo Isaka ambapo pia kitajengwa kiwanda cha kuchenjua madini pamoja na uwepo wa barabara inayoounganisha nchi za maziwa makuu.   “ Kut...

KUPITIA KONGAMANO LA PETROLI LA EAC TUNATAKA NISHATI YA PETROLI IWE INJINI YA MAENDELEO - DKT. MATARAGIO

Image
-Tanzania kuchimba visima vya utafutaji Mafuta Eyasi Wembere* -CNG kufika hadi kwenye mikoa ambayo haijafikiwa na Bomba la Gesi* Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Dkt.James Mataragio amesema Kongamano na Maonesho ya Petroli  ya Afrika Mashariki ( EAPCE'25 ) ambayo yatafanyika Machi 5 hadi 7 mwaka huu jijini Dar es Salaam yanalenga kuhakikisha kuwa nishati ya petroli inakuwa na mchango mkubwa katika kuleta maendeleo kwenye Jumuiya ya Afrika.Mashariki. Amesema hayo tarehe 26 Februari 2025 jijini Dar es Salaam katika Kipindi cha Jambo Tanzania kinachoendeshwa na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) ikiwa ni muendelezo wa programu za kutoa elimu kwa umma kuhusu Kongamano na Maonesho ya 11 ya Petroli ya Afrika Mashariki yatakayofanyika Machi 5-7 mwaka huu. Amesema Tanzania ina rasilimali kubwa ya gesi ambayo iligunduliwa mwaka 1974 Songosongo iliyoanza kuzalishwa mwaka 2004  ambayo inatumika kwenye viwanda, magari, majumbani na kwa kiasi kikubwa inatumika kuzalisha umeme. Ame...

CCM YAIONYA ACT KUCHOCHEA FUJO ZANZIBAR

Image
Chama Cha Mapinduzi (CCM )kimekitaka ACT  Wazalendo  kuacha kueneza upotoshaji na kudai kuwa  Uandikishaji wapiga kura  Mikoa wa Kaskazini " A" na 'B'  kuna baadhi ya wananchi hawakuandikishwa.  CCM kimekanusha na kusema  wananchi wote  waliokidhi vigezo kwa vya sheria ya Ukaazi  na majina yao yamo kwenye Daftari la Sheha wa shehia, wote ameandikishwa. Indhari  hiyo imetolewa na Katibu  wa Kamati Maalum ya NEC Zanzibar,   Idara ya Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Mbeto  Khamis  Mbeto , akimkanya Naibu Katibu Mkuu ACT  Wazalendo  Zanzibar,  Omar Ali  Shehe . Mbeto alimtaka Shehe aache kutoa  madai ya kutengeneza kinyume na ukweli dhidi ya watendaji wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC ), Kamati za Ulinzi na Usalama Mikoa , Wilaya  na Makatibu Tawala  SMZ kila wanapotimiza majukumu  yao ya kazi  . 'Shehe   kila wakati  amekuwa kiongozi   kichefuchefu ana...