Posts

Showing posts from June, 2026

MADINI YA YODERITE YATAKIWA KUHIFADHIWA KWA MANUFAA YA VIZAZI VIJAVYO

Image
  📍Dodoma – Kongwa Imeelezwa kuwa kuna umuhimu wa kuchukua hatua madhubuti za kuhifadhi na kulinda madini adimu aina ya Yoderite yanayopatikana katika eneo la Mlima wa Mautia, Wilaya ya Kongwa, Mkoa wa Dodoma, ili kuhakikisha urithi huo wa kipekee wa kijiolojia unabaki salama kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo. Hayo yalisemwa Juni 30, 2026 na Meneja wa Jiolojia kutoka Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST), Solomon Maswi, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari waliotembelea eneo hilo kwa ziara maalumu. Maswi alisema kuwa uhifadhi wa Yoderite unaweza kuiwezesha Tanzania kuwa kitovu cha kimataifa cha tafiti kuhusu madini adimu, sambamba na kuongeza idadi ya watalii wanaotembelea maeneo yenye urithi wa jiolojia. Aliongeza kuwa Yoderite ni miongoni mwa madini adimu yanayoifanya Tanzania kutambulika duniani kutokana na historia yake ya kugunduliwa kwa mara ya kwanza katika Mlima wa Mautia. Aidha, alifafanua kuwa madini hayo yana mchango mkubwa katika tafit...

TANZANIA YAVUTIA UWEKEZAJI WA UJENZI WA VIWANDA VYA KUZALISHA BIDHAA ZA MIGODINI

Image
📍 Dar es salaam Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde leo Juni 30, 2026 amekutana na Mkurugenzi Mkuu na Mmiliki wa Kiwanda cha Kuzalisha Goroli za Chuma “Steel balls” Bw. Hou Songcun kujadiliana juu ya uwekezaji wa Kampuni hiyo nchini ili kuzalisha bidhaa za migodini. Waziri Mavunde amewakaribisha wawekezaji wao kwenye eneo lililotengwa na serikali la Buzwagi Special Economic Zone lililopo wilayani Kahama,Shinyanga kwa ajili ya kujenga kiwanda cha kuzalisha bidhaa za migodini ili kuwahudumia wachimbaji wakubwa na wadogo nchini. Waziri Mavunde amesema serikali ya awamu ya Sita chini ya Uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu imejipanga kuhakikisha inavutia uwekezaji mkubwa kwenye uzalishaji wa bidhaa za migodini ili Tanzania kuwa kitovu za usambazaji wa bidhaa hiyo barani Afrika. “Lengo letu ni kuona wachimbaji wakubwa na wadogo hapa nchini wanapata bidhaa nyingi za kuzalisha madini pasipo kutegemea uagizwaji wa bidhaa hizo kutoka nje ya nchi," amesema Mavunde. Naye, Mmiliki na Mku...

NAIBU WAZIRI MAHUNDI AHIMIZA WANAWAKE KUTUMIA MIKOPO KUINUA UCHUMI,AZINDUA MFUKO WA UWEZO

Image
Na Jackline Minja, Mtwara Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Maryprisca Mahundi, amezindua rasmi Mfuko wa Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi katika Jimbo la Mtwara Mjini (UWEZO Program) na kusema Serikali itaendelea kuunga mkono jitihada za uwezeshaji wa wanawake. Akizungumza katika hafla hiyo Juni 30, 2026, Naibu Waziri Mahundi amesema Serikali inaamini kuwa maendeleo ya Taifa hayawezi kupatikana bila kuyawezeaha makundi maalum wakiwemo wanawake na vijana. Amesema ushiriki wa makundi maalum  katika shughuli za kiuchumi ni hatua ya kujivunia na kuongeza kuwa mafanikio yatapatikana kwa makundi hayo kupatiwa mafunzo stahiki. "Serikali inaamini kuwa maendeleo ya Taifa hayawezi kupatikana bila wananchi wake kuwa na uwezo wa kushiriki kikamilifu katika shughuli za uzalishaji mali na hii ndiyo sababu kuwndelea kuweka mazingira wezeshi kwa wanawake na vijana kupata fursa za kiuchumi kupitia sera na programu mbalimbali," alisema Naibu Waziri Mahund...

WAZIRI MKUU AHIMIZA WATANZANIA KUONGEZA USHIRIKI KATIKA KUWAHUDUMIA WAZEE

Image
Na Jackline Minja WMJWM Dar Es Salaam   Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba amesema umefika wakati kwa Watanzania kuongeza ushiriki wao katika kuwahudumia makundi yenye uhitaji, hususan wazee, kutokana na mabadiliko ya kiuchumi duniani yaliyopunguza utegemezi wa misaada ya wahisani na kuongeza wajibu wa jamii kushiriki katika utoaji wa huduma za kijamii.   Dkt. Mwigulu amesema hayo tarehe 29 Juni, 2026, alipokuwa Mgeni Rasmi katika Hafla ya Kuwaenzi Wazee na Harambee ya Kuchangia Ujenzi wa Kituo cha Wazee cha Petra (Petra Elderly Centre), iliyofanyika katika Hoteli ya Serena, jijini Dar es Salaam.   Amesema Tanzania inaendelea kushuhudia ongezeko la idadi ya wazee kutokana na kuimarika kwa huduma za afya na kuongezeka kwa umri wa kuishi, hali inayohitaji Serikali na wadau mbalimbali kuendelea kuimarisha mifumo ya kuwahudumia wazee.   "Wazee wetu ni hazina ya hekima, busara, maarifa na historia ya Taifa. Tunapaswa kuendelea kuwaheshimu, kuwatunza na kutumia uzoefu wao ka...

UKARABATI WA KITUO CHA KUZALISHA UMEME CHA HALE WAFIKIA ASILIMIA 83 YA UTEKELEZAJI

Image
Na Mwandishi Wetu, Korogwe – Tanga Serikali imeendelea kusimamia utekelezaji wa miradi ya ukarabati wa miundombinu ya umeme nchini, huku Mradi wa Ukarabati wa Kituo cha Kuzalisha Umeme cha Hale wilayani Korogwe, mkoani Tanga, ukifikia asilimia 83 ya utekelezaji. Akikagua maendeleo ya Mradi huo tarehe 29 Juni, 2026 Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi (Mb), amemtaka mkandarasi kuhakikisha anakamilisha kazi ndani ya muda uliopangwa, akisisitiza kuwa Serikali haitakuwa tayari kuongeza muda wa mkataba wa utekelezaji wa mradi huo. Waziri Ndejembi amesema kukamilika kwa ukarabati wa Kituo cha Hale kutaimarisha ufanisi wa uzalishaji wa umeme, kuongeza upatikanaji wa umeme wa uhakika na kuchochea shughuli za kiuchumi katika Mkoa wa Tanga na maeneo ya jirani. “Mkandarasi ahakikishe anakamilisha mradi huu kwa muda uliopangwa ifikapo Julai 31 mwaka huu, ili wananchi waanze kunufaika na huduma ya umeme wa uhakika pamoja na kuimarisha maendeleo ya kiuchumi,” amesema Mhe. Ndejembi. Kwa upande...

DKT MUNISI- PROGRAMU YA TAIFA YA UKUZAJI UJUZI YAENDELEA KUWAJENGA VIJANA

Image
Serikali imeendelea kudhihirisha dhamira thabiti ya kuwawezesha vijana kiujuzi kupitia Programu ya Taifa ya Ukuzaji Ujuzi. Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Dkt. Evaline Munisi amesema hayo leo Juni 29, 2026 Mwanza alipotembelea Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Sengerema FDC kwa lengo la kukagua maendeleo ya mafunzo ya Uanagenzi yanayotolewa kupitia programu hiyo. Amesema, Serikali inalenga kujenga nguvukazi yenye ujuzi, maarifa na ubunifu ili kukidhi mahitaji ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 na kuongeza ushindani katika soko la ajira la ndani na nje ya nchi. Dkt. Munisi alisema Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano inaendelea kutekeleza Programu ya Taifa ya Kukuza Ujuzi kwa kushirikiana na sekta binafsi kupitia mfumo wa ubia (PPP), huku mafunzo ya uanagenzi yakichukua nafasi muhimu katika kuziba pengo la ujuzi kwa vijana.  Vile vile, amesema kuwa mfumo huo unamwezesha mwanagenzi kutumia asilimia 40 ya muda kujifunza nadharia ...

MSAJILI WA HAZINA AONYA TAASISI ZA UMMA ZENYE UTENDAJI DUNI

Image
Dar es Salaam. Serikali imeonya taasisi za umma zinazofanya vibaya kujitathmini na kuchukua hatua za haraka za kuboresha utendaji wao, ikisisitiza kuwa haitavumilia taasisi zitakazoendelea kuonesha utendaji duni kwa muda mrefu. Onyo hilo lilitolewa na Msajili wa Hazina, Bw. Nehemiah Mchechu, jijini Dar es Salaam Ijumaa, Juni 26, 2026, wakati wa mahojiano maalumu kuelekea Siku ya Gawio itakayofanyika Jumanne, Juni 30, 2026, katika Ikulu ya Dar es Salaam. Bw. Mchechu alisema taasisi zote zinazostahili kuwasilisha gawio na michango mingine Serikalini zinapaswa kutekeleza wajibu huo kwa wakati, akisisitiza kuwa kushindwa kufanya hivyo ni kuinyima Serikali na wananchi mapato stahiki. “Mashirika si mali ya bodi za wakurugenzi wala menejimenti; ni mali ya umma zinazosimamiwa na Serikali. Kwa muktadha huo, kurejesha kilicho haki ya wananchi si fadhila, bali ni wajibu,” alionya. Alisisitiza kuwa viongozi wa taasisi za umma wanapaswa kuhakikisha malengo ya faida wanayopewa yanafikiwa ili kuongez...

TANESCO YAELEZA SABABU YA KUKATIKA KWA UMEME, UREJESHAJI WAANZA KWA AWAMU

Image
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linautaarifu umma kuwa leo Juni 27, 2026, majira ya saa 1:00 usiku, kumetokea hitilafu ya kiufundi katika Mfumo wa Gridi ya Taifa ya umeme, hali iliyosababisha mikoa yote inayopata huduma kupitia gridi hiyo kukosa umeme. Shirika hilo linaendelea na jitihada za kurejesha huduma ya umeme kwa awamu katika maeneo yaliyoathirika ili kuhakikisha huduma inarejea katika hali ya kawaida. Aidha, TANESCO imewaomba radhi wananchi kwa usumbufu uliojitokeza na kuwashukuru kwa uvumilivu wao wakati kazi za kurejesha huduma zikiendelea.

RAIS DKT. SAMIA KUFUNGUA MKUTANO MKUBWA WA MADINI NOVEMBA 2026

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. Samia S. Hassan anatarajiwa kufungua rasmi Mkutano wa Saba wa Madini na Uwekezaji Tanzania (TMIC 2026) utakaofanyika Novemba 19 hadi 21, 2026 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), Dar es Salaam. Akizungumza leo Juni 27, 2026 wakati wa uzinduzi wa TMIC 2026, Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, amesema serikali imeamua kujenga uchumi wa viwanda unaotokana na madini kwa kuwekeza katika uchakataji na uyeyushaji wa madini badala ya kuendelea kuuza malighafi. Amesema kaulimbiu ya mkutano huo, "Madini Yaliyoongezwa Thamani: Chachu ya Ukuaji wa Viwanda na Uchumi," inaakisi dira ya serikali ya kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha uchakataji wa madini barani Afrika. Kwa mujibu wa Mhe. Mavunde, amesema Tanzania tayari ina viwanda vinane vya kusafisha dhahabu, huku Mkoa wa Dodoma ukiwa na viwanda tisa vinavyojengwa na vinavyoendelea na uzalishaji pamoja na kiwanda kikubwa cha kuyeyusha madini ya nikeli na shaba. ...

CUF-ZUIO LA MIKUTANO YA HADHARA KWA VYAMA VYA SIASA NI HARAMU NA HALIKUBALIKI

Image
CUF- Chama Cha Wananchi tumepokea taarifa ya kupigwa marufuku kwa mikutano ya HADHARA kwa Vyama vya Siasa kwa mshangao na masikitiko makubwa.  Kauli iliyotolewa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi kuhusu kuzuia mikutano ya hadhara kwa vyama vya Siasa haikubaliki na kwa vyovyote vile ni kichocheo kingine cha vurugu katika kipindi hiki ambapo bado Taifa linaugulia ya majeraha yaliyotokana na vurugu na Mauaji ya Oktoba 29, 2025. Mapema mwaka 2024 Dkt Samia Suluhu Hassan akiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kufuatia kifo cha Rais Dkt  John Pombe Magufuli aliweka bayana kwamba Mikutano ya hadhara kwa vyama vya Siasa ni Haki ya Kikatiba na Kisheria, hivyo kuizuia haikuwa sawa. Tunamkumbusha Waziri Katambi kwamba kwa vyovyote vile sauti yake haipaswi kupanda juu ya Sauti ya Mteuzi wake na kwamba Katiba na Sheria alizozirejea Dkt Samia Suluhu Hassan mwaka 2024 havijabadilika. Kupitia mabadiliko ya wakati, CUF- Chama Cha Wananchi kiliitahadharisha Serikali ya Awamu ya tano kut...

SERIKALI YAENDELEA KUCHUKUA HATUA KUIMARISHA HUDUMA ZA USTAWI WA JAMII KWA WATOTO

Image
Na Jackline Minja, WMJWM Dodoma Serikali imeendelea kuchukua hatua za kuimarisha ustawi wa watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi kwa kuratibu vikao shirikishi vya kijamii vinavyowapa elimu wazazi na walezi kuhusu wajibu wao wa malezi, matunzo na ulinzi wa watoto, hususan yatima na watoto wenye ulemavu.  Hayo yameelezwa na  Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima, Bungeni jijini Dodoma leo, Juni 26, 2026, alipokuwa akijibu hoja mbalimbali za wabunge. Waziri Dkt. Gwajima amewataka wazazi kutoruhusu migogoro yao ya kifamilia kuwa chanzo cha watoto kukosa malezi na kuishia kuishi mitaani katika mazingira hatarishi.  "Wazazi niwasihi pale ambapo migogoro ya wazazi itakuwa imefikia hatua ya kushindwa kuwalea watoto kwa wakati, ni vyema mkakawapeleka watoto hao katika vituo vya ustawi wa jamii ili wapate malezi na ulinzi stahiki kwa muda, badala ya kuwaacha wakitelekezwa." amesema Dkt. Gwajima Akijibu swali la msingi...