DKT. NCHEMBA AWAKARIBISHA WAWEKEZAJI MRADI WA SGR
Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), ameishukuru Benki ya Maendeleo ya Afrika Kusini (DBSA), kwa kushiriki katika ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR), mradi ambao ni muhimu kwa uchumi wa Tanzania na nchi jirani zitakazonufaika na mnyororo wa thamani wa mradi huo wa kikanda. Mhe. Dkt. Nchemba amesema hayo alipokutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Bi. Buitumelo Mosako, kando ya Mikutano ya Mwaka ya Bodi ya Magavana wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) iliyofanyika, Abidjan nchini Ivory Coast. “Tunapenda kutoa shukrani zetu za dhati kwa Benki ya Maendeleo ya Afrika Kusini (DBSA) kwa mchango wenu muhimu katika kufadhili ujenzi wa SGR kipande cha 3 na 4 (Makutupora hadi Isaka) kwa kiasi cha dola za Marekani milioni 100. Zaidi ya hapo, tunatambua na kuthamini msaada wa kifedha wa kiasi cha dola milioni 100 uliotolewa awali kwa ajili ya kujenga kipande cha 2, ambao uliweka msingi imara kwa mradi mzima wa SGR” alisema Dkt. Nchemba Alisema kuwa kuto...