Posts

Showing posts from February, 2026

KAMATI YA UONGOZI WA MRADI WA JNHPP YAKAGUA MAENDELEO YA BWAWA LA JULIUS NYERERE

Image
Kamati ya Uongozi wa Mradi wa Bwawa la Julius Nyerere (JNHPP), tarehe 26 Februari 2026, imekagua maendeleo ya uzalishaji wa umeme katika mradi huo na kueleza kuridhishwa na usimamizi pamoja na utekelezaji wake, uliokidhi viwango vya ubora vinavyoendana na thamani ya fedha iliyowekezwa na Serikali. Mwenyekiti wa Kamati hiyo, ambaye pia ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Dkt. Jim Yonazi , amesema kamati imefurahishwa na namna bwawa hilo linavyochochea ukuaji wa uchumi kwa kuongeza uzalishaji wa umeme unaosambazwa katika maeneo mbalimbali nchini, hatua inayochangia kuimarika kwa upatikanaji wa nishati ya umeme. “Tumeridhishwa na jinsi mradi huu ulivyosimamiwa na kutekelezwa kwa ufanisi mkubwa. Ukilinganisha na miradi mingine barani Afrika, mradi huu umejengwa kwa ubora wa hali ya juu na umeleta unafuu katika huduma ya umeme nchini. Haya ni mafanikio makubwa kwa Taifa,” alieleza Dkt. Yonazi. Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishat...

WANANCHI PERAMIHO, SHIWINGA KUPIGA KURA KESHO KUCHAGUA MBUNGE, DIWANI

Image
 Na Mwandishi wetu, Ruvuma Wapiga Kura 127,632 walioandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura watashiriki katika uchaguzi wa kuchagua Mbunge katika Jimbo la Peramiho lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Mkoa wa Ruvuma na Kata ya Shiwinga iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi Mkoa wa Songwe.   Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele ameyasema hayo leo Februari 25, 2026 mjini Songea Mkoani Ruvuma wakati akisoma risala maalum kuhusu uchaguzi katika jimbo na kata husika utakao fanyika kesho Februari 26, 2026 na kusema kuwa jumla ya vituo 373 vya Kupigia Kura vitatumika.   “Kati yao wapiga kura 120,780 ni wa Jimbo la Peramiho na wapiga kura 6,852 wapo katika kata ya shiwinga na jumla ya vituo 373 vya Kupigia Kura vitatumika, ambapo vituo 354 vipo Jimbo la Peramiho na vituo 19 vipo katika Kata ya Shiwinga Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi,”amesema Jaji Mwambegele.   Aidha, amesema kwa uchaguzi mdogo wa ubunge Jimbo la ...

INEC YAWAFUNDA WASIMAMIZI NA WASIMAMIZI WA SAIDIZI WA VITUO VYA KURA JIMBO LA PERAMIHO

Image
  Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Mhe. Jaji wa Rufaa Jacobs Mwambegele leo Februari 23, 2026 ametembelea mafunzo ya Wasimamizi na Wasimamizi Wasaidizi ngazi ya vituo katika Jimbo la Peramiho lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma na kuzungumza nao ambapo amewasisitiza kutekeleza majukumu yao kwa weledi kwa kufuata Sheria, Kanuni na maelekezo ya Tume. Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Mhe. Jaji wa Rufaa Jacobs Mwambegele leo Februari 23, 2026 ametembelea mafunzo ya Wasimamizi na Wasimamizi Wasaidizi ngazi ya vituo katika Jimbo la Peramiho lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma na kuzungumza nao ambapo amewasisitiza kutekeleza majukumu yao kwa weledi kwa kufuata Sheria, Kanuni na maelekezo ya Tume. Mafunzo hayo ya siku mbili yalifanyika katika Kumbi tatu tofauti za  Seminari Kuu Peramiho, Maposeni Sekondari na Ukumbi wa Josephat Mkuwa  ni maandalizi ya Uchaguzi Mdogo wa Ubunge katika Jimbo la Peramiho a...

INEC YAWAPIGA MSASA MAKARANI WAONGOZAJI WAPIGA KURA PERAMIHO, SHIWINGA

Image
  Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Mhe. Jaji wa Rufaa Jacobs Mwambegele akizungumza leo Februari 22, 2026 na washiriki wa mafunzo ya makarani waongozaji wapiga kura kwa ajili ya Uchaguzi mdogo wa Jimbo la Peramiho unaotarajiwa kufanyika tarehe 26 Februari, 2026.  Na Waandishi wetu, Ruvuma na Songwe Tume huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imewataka Makarani Waongozaji wapiga kura katika Jimbo la Peramiho lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma kutekeleza majukumu yao bila woga kwa kufuata Sheria, Kanuni, maelekezo ya Tume.   Wito huo umetolewa na  Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Mhe. Jaji wa Rufaa Jacobs Mwambegele leo Februari 22, 2026 wakati akizungumza na washiriki wa mafunzo ya makarani waongozaji wapiga kura kwa ajili ya Uchaguzi mdogo wa Jimbo la Peramiho unaotarajiwa kufanyika tarehe 26 Februari, 2026.  “Nawasihi mnapokwenda kufanya kazi yenu mkawe wakarimu na wanyenyekevu katika kutekeleza shughuli zen...

TANZANIA YAANDIKA HISTORIA MPYA: MRADI WA UMEME JUA KISHAPU WAKAMILIKA

Image
Tanzania imeandika historia mpya katika sekta ya nishati baada ya kukamilika kwa ujenzi wa Mradi wa Kuzalisha Umeme kwa nishati ya jua ulioko Kishapu, mkoani Shinyanga mradi ambao ni mkubwa na wa kwanza wa aina yake nchini. Akizungumza Februari 21, 2026 mara baada ya kukagua maendeleo ya mradi huo, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Bw. Lazaro Twange, amesema kukamilika kwa mradi huo ni ushahidi wa dhamira thabiti ya Serikali ya Awamu ya Sita katika kuimarisha upatikanaji wa huduma ya umeme ya uhakika kwa Watanzania. “Hii ni historia mpya imeandikwa kwa nchi yetu. Tangu tupate uhuru, hatujawahi kuwa na mradi mkubwa wa aina hii ya umeme wa jua. Serikali kupitia Wizara ya Nishati na TANESCO imeandika historia, na leo mmeshuhudia hapa umeme ukizalishwa. Mpaka kufikia Machi 1, 2026 jumla ya Megawati 50 zitakuwa zimeunganishwa kwenye Gridi ya umeme ya Taifa,” alisisitiza Bw. Twange. Bw. Twange ametumia fursa hiyo kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan...

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO

Image
 

CARDINAL PENGO AFARIKI DUNIA

Image
Askofu Mkuu wa Dar-es-Salaam Thaddeus Ruwa’ichi kwa masikitiko makubwa ametangaza kifo cha Mwadhama Polycarp Cardinal Pengo, Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo kuu la Dar-es-Salaam. Kifo cha Cardinal Pengo kimetokea akiwa katika taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) Dar-es-Salaam.

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO

Image

MAKAMU MWENYEKITI INEC NA WAJUMBE WA TUME WAMTEMBELEA RC SONGWE

Image
Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani (Mst) Mbarouk Salim Mbarouk leo Februari 19, 2026 akiwa na Mjumbe wa Tume, Mhe. Dkt. Zakia Mohamed Abubakar wamemtembelea  ofisini kwake Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Jabiri Omari Makame.  Viongozi hao wa Tume wapo mkoani humo kwa ziara ya kikazi ambapo wametembelea na kukagua maandalizi ya Uchaguzi mdogo wa Udiwani Kata ya Shiwinga, Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, Mkoani Songwe unaotarajiwa kufanyika Februari 26, 2026.

PROF. SHEMDOE, MENEJIMENTI LUSHOTO WAKUTANA KUJIPANGA KUTEKELEZA MAELEKEZO YA WAZIRI MKUU

Image
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu -TAMISEMI Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amefanya kikao kazi na Menejimenti ya Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto, kilicholenga kuweka mkakati wa utekelezaji wa maelekezo ya Mhe. Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba hususani ya utatuzi wa kero na changamoto za wananchi, aliyoyatoa Februari 17, 2026 wakati wa ziara yake wilayani Lushoto.  Katika kikao kazi hicho kilichofanyika Feberuari 18, 2026 katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto, Prof. Shemdoe ameisisitiza Menejimenti ya Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto kuhakikisha inasimamia  kikamilifu utatuzi wa kero na changamoto zinazowakabili wananchi kama alivyoelekeza Mhe. Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba. "Mmemsikia Mheshimiwa Waziri Mkuu akituasa tubadilike kiutendaji, tuachane na utendaji kazi wa mazoea hivyo twendeni tukasikilize kero na changamoto zinazowakabili wananchi na tuzitatue kwa wakati," amesisitiza Prof. Shemdoe. Prof. Shemdoe amefafanua kuwa, ufanyaji kazi wa mazoea ...

BWEGE AHAMIA CHADEMA

Image
 Aliyewahi kuwa Mbunge wa Kilwa Kunisini, Selemani Said Ally maarufu "Bwege"  ametangaza rasmi kujivua uanachama wa chama cha ACT WAZALENDO. Katika taarifa yake aliyoitoa, Bwege ameeleza kuwa uamuzi huo umetokana na Hiari yake mwenyewe kutoka moyoni , baada ya kutafakari kwa muda mrefu na kugundua kuwa ACT WAZALENDO sio rafiki sahihi kwake.

SERIKALI YAZINDUA AWAMU YA KWANZA YA MRADI WA KUPELEKA NISHATI SAFI YA KUPIKIA KWA TAASISI ZINAZOHUDUMIA WATU ZAIDI YA 100

Image
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba,  amezindua awamu ya kwanza ya mradi wa kusambaza nishati safi ya kupikia katika taasisi zinazohudumia watu zaidi ya 100, unaohusisha shule 52 za sekondari pamoja na chuo kimoja cha Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) katika mikoa 18 ya Tanzania Bara. Mradi huo ni sehemu ya mpango mkubwa wa kuunganisha miundombinu ya nishati safi ya kupikia katika taasisi 453 wenye thamani ya Shilingi bilioni 25.8, ambapo gharama zote zinagharamiwa kwa asilimia 100 na Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA).  Mhe. Salome Makamba amezindua mradi huo tarehe 17 Februari 2026 katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Kondoa, mkoani Dodoma, ambayo imekuwa taasisi ya kwanza kufungiwa mfumo wa nishati safi ya kupikia kupitia mradi husika. Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mhe. Salome amesema  kuwa mradi unahusisha usimikaji wa mifumo ya gesi ya LPG, ufungaji wa majiko banifu  pamoja na usambazaji wa mkaa mbadala katika taasisi 453. Ameeleza k...