TMA YAWAPA TAHADHARI WAKULIMA,WAFUGAJI
Wakulima na Wafugaji Nchini wameshauriwa kutumia taarifa sahihi kutoka kwa maafisa ugani kwa kuzingatia utabiri wa wilaya husika katika kuchagua mbegu na zao sahihi kulingana na utabiri wa msimu. Wito huo umetolewa leo Oktoba 31,2024 Jijini Dar es salaam na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Sayansi ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Tabianchi (IPCC), Dkt. Ladislaus Chang'a wakati akitoa taarifa ya mwelekeo wa mvua za Msimu wa Novemba, 2024 hadi Aprili 2025. Amesema kuwa Mvua hizo zimeanza katika baadhi ya maeneo ya ukanda wa Ziwa Victoria na pwani ya kaskazini kama ilivyotabiriwa nakwamba maeneo ya nyanda za juu kaskazini mashariki yameendelea kutawaliwa na vipindi virefu vya ukavu. Aidha,meendelea kufafanua kuwa utabiri wa mvua za Vuli unatarajiwa kuendelea kama ulivyotabiriwa ambapo Mwelekeo wa mvua za Msimu wa Novemba, 2024 hadi Aprili, 2025, Mvua hizo ni mahususi katika maeneo ya ma...