Posts

Showing posts from January, 2026

MATOKEO YA MTIHANI KIDATO CHA NNE 2025 HAYA HAPA

Image
BOFYA KUTAZAMA MATOKEO BOFYA KUTAZAMA MATOKEO

RAIS SAMIA AMEJIPANGA KUFIKISHA UMEME VITONGOJI VYOTE

Image
📍Njombe Imeelezwa kuwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameelekeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA), kufikisha umeme kwenye vitongoji vyote vilivyobakia nchini ambavyo bado havina huduma ya umeme ifikapo mwaka 2030. Hayo yamebainishwa leo Januari 30, 2026 na Bw. Frank Mugogo kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mha. Hassan Saidy wakati wa hafla fupi ya kumtambulisha mkandarasi kutoka kampuni ya Central Electricals International Ltd katika Mradi wa HEP 2B ambaye anaenda kutekeleza kwenye vitongoji 218 mkoani Njombe. "Jumla ya vitongoji vyote mkoa wa Njombe ni 1,833 na vitongoji vyenye umeme ni 1,276. Vilevile vitongoji ambavyo havina umeme ni 557. Hivyo mradi huu unakwenda kupeleka umeme kwenye vitongoji 218 katika mkoa huu na vitabakia vitongoji 339 ambavyo havina umeme navyo vitakamilika, " Amesema Bw. Mugogo. Ameongeza kuwa, gharama za kuunganisha umeme huo ni shilingi 27,000 tu na kuwataka wananchi wa mkoa huo kutumia fursa ya kuunga...

SERIKALI YAKARIBISHA KAMPUNI ZA KOREA KUSINI KUWEKEZA SEKTA YA MADINI

Image
Katika hatua ya Tanzania kuendelea kujiimarisha kama kitovu cha uwekezaji wa kimkakati barani Afrika, Serikali kupitia wizara ya madini imekaribisha uwekezaji wa Kampuni kutoka Korea Kusini kuja kuwekeza nchini na kueleza uwepo wa fursa katika utafiti wa madini, uongezaji thamani pamoja teknolojia za kisasa za uchimbaji na uchakataji madini hususan madini muhimu na mkakati. Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Msafiri Mbibo, Amesema hayo Januari 28, 2026 Jijini Dodoma wakati akizungumza na ujumbe kutoka Korea Kusini ukijumuisha Shirika la Kukuza Biashara na Uwekezaji la Jamhuri ya Korea (Korea Trade-Investment Promotion Agency – KOTRA) na Kampuni ya HD Construction Equipment kutoka nchini Korea Kusini inayojihusisha na utengenezaji wa vifaa na teknolojia ya uchimbaji na viwanda. Mbibo alisisitiza kuwa Sera na maboresho ya kisheria yaliyofanywa na Serikali ya Tanzania katika Sekta ya Madini yamelenga kuvutia mitaji yenye teknolojia, maarifa, na mtazamo wa muda mrefu, hasa katika uchak...

MUCOHAS, WIZARA YA AFYA, MUHAS ZATEKELEZA MRADI WA AFUA JUMUISHI KUBORESHA HUDUMA RAFIKI KWA WAGONJWA WA VVU NA WATUMIAJI DAWA ZA KULEVYA

Image
Chuo cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUCOHAS) kwa kushirikiana Wizara ya Afya na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi (MUHAS), zinaendelea kutekeleza mradi wa Afua Jumuishi (Total Facility Approach) unaolenga kuondoa unyanyapaa na ubaguzi miongoni mwa watoa huduma za afya kwa wagonjwa wanaoishi na Virusi vya Ukimwi (VVU) pamoja na watumiaji wa dawa za kulevya.  Kikao cha siku tano kinafanyika mkoani Morogoro, kikilenga kuandaa nyenzo za  kufundishia ili kuwajengea uwezo walimu  na wanafunzi wa vyuo vya kati, juu ya unyanyapaa na ubaguzi. Akizungumza kuhusu utekelezaji wa mradi huo, Mkuu wa Chuo cha MUCOHAS, Dkt. Bonny Betson, amesema mradi huo umejikita katika kuboresha uelewa, mitazamo na ujuzi wa watoa huduma ili kuhakikisha huduma za afya zinazotolewa ni jumuishi, rafiki na zenye kuzingatia utu wa kila mteja. “Huu ni mwaka wa tatu tangu tulipoanza mradi huu, na kwa sasa tumetekeleza awamu ya kwanza hapa MUCOHAS kwa wanafunzi na walimu, baada ya hapo tuna...

TANESCO YAFANYA UKAGUZI WA MITA KUBAINI MALALAMIKO YA UMEME KUISHA HARAKA

Image
NA MWANDISHI WETU SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) limefanya ukaguzi wa kitaalamu wa mita za umeme kwa baadhi ya wateja waliowasilisha malalamiko hayo kwa njia za mitandao katika maeneo ya Tabata Kimanga na Kimara Suka jijini Dar es Salaam. Malalamiko hayo yaliibuliwa na baadhi ya wananchi mitandaoni na kwenye vyombo vya habari kuhusu madai ya umeme kuisha haraka bila sababu ya msingi. Zoezi hilo lilifanyika Januari 27, 2026, likiongozwa na Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano na Huduma kwa Wateja wa TANESCO, Bi. Irene Gowelle, akiambatana na timu ya wataalamu wa Shirika, kwa lengo la kubaini chanzo halisi cha changamoto hiyo na kujiridhisha kuhusu ufanisi wa utendaji wa mita za wateja. Matokeo ya Ukaguzi Baada ya kufanyiwa vipimo vya kitaalamu, TANESCO imebaini kuwa mita zote zilizokaguliwa zilikuwa salama na zinafanya kazi kwa usahihi, kinyume na madai yaliyokuwa yakitolewa kuwa mita hizo zina kasoro ya kiutendaji. Hata hivyo, ukaguzi umeonesha kuwa vyanzo vilivyopelekea wateja walioka...

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO

Image
 

TWIGA, TANGA CEMENT WAPEWA SAA 48 KUJISALIMISHA

Image
Serikali kupitia Wizara ya Madini imezipa Kampuni za Twiga Cement na Tanga Cement saa 48 kufika mbele ya mamlaka husika na kujibu hoja zinazowakabili, ikiwemo madai ya kukiuka bei elekezi za madini zinazotolewa na Serikali na kukosa mikataba kwa wauzaji wa malighafi viwandani. Akizungumza leo katika kikao cha wachimbaji wadogo wa madini ya Jasi (gypsum) kutoka Same mkoani Kilimanjaro kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Gold, Ofisi za Tume ya Madini jijini Dodoma, Naibu Waziri wa Madini, Mhe. Dkt. Steven Kiruswa, amesema kampuni hizo zikikaidi wito huo, Serikali itachukua hatua kali ikiwemo kusimamisha shughuli zao. “Kitendo cha kukaidi wito wa Serikali ni kuidharau mamlaka. Wasipofika ndani ya saa 48, tutamshauri Waziri kufuta leseni zao,” amesema Mhe. Dkt. Kiruswa. Amesisitiza kuwa kampuni hizo zinapaswa kulipa wasambazaji wa madini ya jasi kwa kuzingatia bei elekezi iliyowekwa na Serikali, kutoa mikataba ya kazi kwa wauzaji wa bidhaa, na kuacha kununua kwa bei ya chini inayowaumiza wachi...

WATENDAJI WA UCHAGUZI WATAKIWA KUTEKELEZA MAJUKUMU KWA WELEDI

Image
Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufaa (Mstaafu) Mbarouk Salim Mbarouk akizungumza leo tarehe 26 Januari, 2026 mkoani Iringa wakati akifunga mafunzo ya siku tatu ya watendaji wa uchaguzi kutoka Halmashauri za Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma na Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, mkoani Songwe.(Picha na INEC). Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufaa (Mstaafu) Mbarouk Salim Mbarouk akizungumza leo tarehe 26 Januari, 2026 mkoani Iringa wakati akifunga mafunzo ya siku tatu ya watendaji wa uchaguzi kutoka Halmashauri za Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma na Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, mkoani Songwe. Meza Kuu ikiongozwa na Mwenyekiti wa Tume, Jaji wa Rufaa Jacobs Mwambegele ikiwa katika ufungaji wa mafunzo hayo. Washiriki wa mafunzo ya watendaji wa uchaguzi kutoka Halmashauri za Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma na Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, mkoani Songwe wakifuatilia hotuba ya ufungaji mafunzo yao ya siku tatu. Washiriki wa ma...

NISHATI SAFI YA RAFIKI BRIQUETTES IWAFIKIE WATANZANIA WOTE - BALOZI KINGU

Image
  Watanzania wametakiwa kuendelea kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kutumia nishati safi ya kupikia (mkaa mbadala wa Rafiki briquettes) unaozalishwa na Shirika la Madini la Taifa (STAMICO).  Rai hiyo imetolewa leo Januari 24, 2026 na Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Meja Jenerali Mstaafu Mhe. Balozi Jacob Kingu akiwa ameambatana na Wajumbe wa REB na Menejimenti ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) walipotembelea kiwanda cha Nishati safi ya Rafiki Briquettes kinachomilikiwa na STAMICO kilichopo Kisarawe Mkoani Pwani. Balozi Kingu amewataka STAMICO kuongeza kasi ya uzalishaji wa mkaa wa Rafiki briquettes ili watanzani wote nchini waweze kutumia nishati safi ya kupikia na salama.  “Hii ajenda ya matumizi ya nishati safi ambayo kinara wake ni Rais wa Awamu ya Sita, Dkt. Samia Suluhu Hassan inalenga kumkomboa Mwanamke ili aachane na matumizi ya nishati isiyo safi na salama. Tunahamasisha na kutekeleza maono...

WATUMISHI WIZARA YA MADINI NA TAASISI ZAKE WAHAMASISHWA KUFANYA MAZOEZI

Image
Watumishi wa Wizara ya Madini na Taasisi zake wamehimizwa kufanya mazoezi ya mwili mara kwa mara kama njia ya kuimarisha afya, kujenga mshikamano na kuongeza tija katika utekelezaji wa majukumu ya kazi. Wito huo umetolewa leo Januari 24, 2026 jijini Dodoma na Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde, alipofungua Bonanza la tatu la michezo lililowakutanisha watumishi wa Wizara ya Madini na Taasisi zake, ikiwemo Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST), Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), Tume ya Madini pamoja na Taasisi ya Uwazi na Uwajibikaji katika Rasilimali Madini, Mafuta na Gesi Asilia (TEITI).  Akizungumza katika uzinduzi wa bonanza hilo, Mhe. Mavunde amesema kuwa,  mazoezi ya viungo ni nguzo muhimu ya afya njema kwa mtumishi, ufanisi na tija kazini hivyo kuna  umuhimu wa watumishi kujitokeza kwa wingi katika shughuli za michezo ili kuimarisha afya zao na kuendeleza mshikamano kazini. Aidha, Waziri Mavunde amezitaka taasisi zote zilizo chini ya Wizara ...