Posts

Showing posts from March, 2025

JKI YATOA MKONO WA IDDI KWA WENYE UHITAJI KIPUNGUNI, ILALA

Image
****** Taasisi ya isiyo ya Kiserikali ya Jamii Kwanza initiative (JKI) kwa Kushirikiana na Ofisi ya Serikali ya Mtaa wa Amani Kata ya Kipunguni,Ilala Jijini Dar es salaam Leo Machi 29,2025 imefanikisha kutoa mkono wa Iddi kwa watu wenye uhitaji wakiwemo Yatima na Wajane ili waweze kusherehekea sikukuu ya Eid El Fitri inayotarajiwa siku ya Jumatatu inategemea na kuandama kwa mwezi. Akizungumza mara baada ya kugawa sadaka hiyo Mkurugenzi wa JKI Daniel Migera amesema kuwa kitendo walichokifanya ni moja ya jukumu lao kama Taasisi kurejesha kwa Jamii shukurani na kudumisha amani,upendo na furaha. "Tumeamua kunyoosha mkono ili kudumisha amani na Umoja,tumetoa swadaka hiyo ili Kuwawezesha na wao kufurahia hii muhimu kwao mara baada ya kumaliza Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani " Amesema Migera. Bw. Migera ametoa Rai kwa Taasisi zingine wakiwemo Wadau mbalimbali, watu wenye Uwezo kuwasaidia wenye uhitaji Maalum kwani kufanya jambo kama hilo ni muhimu kwa kujenga amani,Umoja, mshik...

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO

Image

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO

Image

TANESCO YASHINDA TENA TUZO ZA UBORA HUDUMA KWA WATEJA ZA CICM

Image
Shirika la umeme Tanzania TANESCO kwa mara nyingine tena limeshinda tuzo ya the ''Most improved Organization'' eneo la huduma kwa wateja iliyotolewa na Taasisi ya Chartered Institute of Customer Management(CICM). Tuzo hizo zimetolewa  28, Machi 2025 jijini Dar es Salaam ambapo Shirika limepata tuzo hiyo baada ya kufanya maboresho ya kutumia njia za kidigitali kurahisisha mchakato wa maombi ya umeme na upatikanaji wa huduma kuwa mwepesi kwa wateja wake. Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO , Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano na Huduma kwa Wateja Bi  Irene Gowelle  amesema Tuzo hizo ni heshima kwa Shirika ikiwa ni ishara nzuri ya maboresho yanayofanyika kutambuliwa na kuthaminiwa. ‘’ Tuzo hizi ni heshima kubwa kwa TANESCO, zinatuongezea ari ya kufanya vizuri zaidi,tutaongeza ubunifu katika utoaji wa huduma bora kwa wateja wetu’’ Aidha , Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO Mha. Gissima Nyamo-Hanga na yeye alishinda Tuzo ya heshima ya Kiongozi anayefanya mabadil...

MATARAJIO YA HALI YA HEWA KWA SIKU 5

Image

WASIRA: CHADEMA HAWANA HOJA YA MSINGI KUZUIA UCHAGUZI MKUU

Image
  Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira amesema Chama cha Demokrasia na Maendeleo hakina hoja ya msingi kuzuia uchaguzi mkuu wa mwaka huu kwa kuwa malalamiko ya kutaka mabadiliko wanayoyazungumza yameshafanyika. Amesema CHADEMA inadai haitashiriki uchaguzi hadi yafanyike mabadiliko ya kisheria yakiwemo ya uchaguzi, hata hivyo mabadiliko hayo yameshafanyika. Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika eneo la Stendi katika Halmashauri ya Wilaya ya Kahama, Wasira alisema sheria zilizofanyiwa mabadiliko ni pamoja na Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na madiwani. Alisema nyingine ni Sheria ya Tume ya Uchaguzi pamoja na Sheria ya Vyama vya Siasa vinavyosimamiwa na msajili wa vyama vya siasa na kuongeza mambo hayo ndiyo waliyokuwa wakiyalalamikia. “Moja wanasema wao hawataki uchaguzi wanasema tume ile inateuliwa na Rais moja kwa moja kwa hiyo sio huru, tukasema hamna tabu, wabunge wakaunda kwamba tuweke kamati maalumu ili mtu anayetaka ukami...

TANZANIA NA UNOPS ZAENDELEA KUIMARISHA USHIRIKIANO KATIKA MIRADI YA MAENDELEO

Image
  Dar es Salaam, 28 Machi 2025 – Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel William Shelukindo, amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Kanda ya Mashariki na Kusini mwa Afrika wa Ofisi za Umoja wa Mataifa za Huduma za Miradi (UNOPS), Bw. Rainer Frauenfeld, aliyefuatana na ujumbe wake. Katika mazungumzo hayo, Balozi Shelukindo amepongeza ushirikiano mzuri kati ya Serikali ya Tanzania na UNOPS katika kusaidia utekelezaji wa miradi ya maendeleo nchini. Amesisitiza kuwa Tanzania inathamini mchango wa UNOPS katika sekta mbalimbali, hususan miundombinu ya barabara na huduma za kijamii, ambazo zimekuwa na mchango mkubwa katika kuinua uchumi wa Taifa na kuboresha maisha ya wananchi. Aidha, Balozi Shelukindo ameweka bayana dhamira ya Serikali kuendelea kushirikiana na UNOPS ili kuhakikisha miradi inayotekelezwa inazidi kuleta tija na kuendana na vipaumbele vya maendeleo vya Taifa. Pia, amesisitiza umuhimu wa kuimarisha mifumo ya ute...

SERIKALI YAAGIZA MAGEREZA KUPEWA RUZUKU YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

Image
-Dkt. Biteko atoa mabati 300 ujenzi wa darasa Chuo cha Mafunzo - Magereza yapongezwa kutumia Nishati Safi ya Kupikia - Dkt. Samia apongezwa kwa kuimarisha vyombo vya ulinzi na usalama Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ameilekeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kutoa ruzuku kwa Jeshi la Magereza ili kutekeleza maelekezo ya Serikali kuhusu matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia na kuhakikisha  Magereza yote yanaondokana na Nishati isiyo safi. Dkt. Biteko ametoa agizo hilo leo Machi 28, 2025 jijini Dar es salaam katika hafla ya kufunga Mafunzo ya Uongozi  Ngazi ya Juu  Namba 27 - 2024/2025  katika Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji Tanzania (TCTA). “ Magereza yote 129 yamehama katika matumizi ya kuni na sasa yanatumia nishati safi ya kupikia. Naielekeza REA ile ruzuku tunayopanga kuitoa kwa wazalishaji mbalimbali kwa ajili ya vifaa  vya matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia Magereza wapewe kip...