Posts

Showing posts from October, 2025

WAPIGA KURA 37,647,235 KUPIGA KURA KATIKA UCHAGUZI MKUU OKTOBA 29

Image
  Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akizungumza na wananchi wakati akisoma risala yake kuhusu Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani unaotaraji kufanyika Oktoba 29, 2025. 

INEC YAKAGUA VITUO VYA KUPIGIA KURA JIMBO LA TANGANYIKA

Image
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele ametembelea na kujionea maandalizi ya ujenzi wa vituo 83 kati ya 90 vya Wapiga Kura vilivyotengwa maalum kwaajili ya wakazi wa zilizokuwa Kata za Ilangu, Ipwaga, Bulamata na Mishamo zilizopo Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika Mkoani Katavi ambazo zilifutwa na Waziri mwenye dhamana ya Serikali za Mitaa kwa mujibu wa Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya), Sura 287. Jaji Mwambegele alitembelea eneo hilo la Kata ya Tongwe katika Kitongoji cha Luhafwe leo Oktoba 26, 2025 akiwa ameambatana na Mratibu wa Uchaguzi Mkoa wa Katavi, Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Tanganyika na watendaji wengine wa uchaguzi kuangalia maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani uliopangwa kufanyika Oktoba 29, 2025 nchini kote. Akizungumza akiwa katika eneo la Mnada wa Kitongoji cha Luhafwe, Jaji Mwambegele alisema Tume ilitangaza kuhamisha baadhi ya vituo nje ya Makazi ya Wakimbizi hivyo amefika na kuangalia ...

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO

Image
 

TUME YATOA MAELEKEZO YA KISERA KATIKA UCHAGUZI MKUU WA MWAKA 2025

Image
   

SERIKALI IMEONESHA DHAMIRA YA DHATI KULINDA MAISHA YETU DHIDI YA MAMBA - WANANCHI MARA,

Image
Na Mwandishi wetu, Mara  Wananchi wa wilaya ya Bunda mkoani Mara wamekiri kuiona dhamira ya dhati ya Serikali inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania - TAWA ya kutatua migongano baina ya wanyamapori na binadamu Kwa kuongeza Idadi ya vizimba, hatua inayotajwa kupunguza athari Kwa wananchi hao. Kauli hiyo imetolewa Oktoba 22, 2025 wakati wa ziara ya kukagua vizimba hivyo ikienda sambamba na utoaji elimu ya kuepuka madhara yanayoweza kusababishwa na wanyampori aina ya mamba na viboko iliyofanywa na maofisa wa TAWA mkoani humo. Miongoni mwa wananchi aliyewahi kujeruhiwa na mamba, Kurwa Ryoba mkazi wa Kijiji cha Buzimbwe  ameishukuru Serikali Kwa hatua hiyo ya kuongeza Idadi ya vizimba akisema vizimba hivyo ni suluhisho muhimu katika kuokoa maisha ya wananchi, huku akiwasisitiza wananchi wenzake kutopuuzia kutumia vizimba hivyo ili wasije wakapata madhara aliyoyapata yeye  "Naish...

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO

Image
 

YANGA YAMFUNGASHIA VIRAGO FOLZ

Image
 

TAMASHA LA NYAMAPORI CHOMA LAVUTA UMATI TABORA ZOO

Image
Na Mwandishi Wetu, TABORA Zaidi ya watalii 500 wamefurika leo, Oktoba 18, 2025, katika Bustani ya Wanyamapori Tabora (Tabora Zoo) kushiriki katika Tamasha la Nyamapori Choma lililoandaliwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) Kanda ya Magharibi. Tamasha hilo lililolenga kuhamasisha utalii wa ndani pamoja na matumizi endelevu na halali ya rasilimali za wanyamapori, limevutia watalii  kutoka maeneo mbalimbali ndani na nje ya nchi, likihudhuriwa na viongozi wa Serikali wakiwemo Wakuu wa Wilaya za Tabora na Uyui, wananchi wa Mkoa wa Tabora na mikoa jirani, pamoja na wageni kutoka mataifa mbalimbali duniani. Wananchi waliohudhuria tamasha hilo wameipongeza TAWA kwa ubunifu wa kuandaa tukio hilo, wakieleza kuwa limewapa fursa ya “kuonja ladha ya matunda ya uhifadhi” unaotekelezwa na Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii Kwa kuhakikisha wananchi wananufaika na rasilimali hizo Kwa njia halali bila kuathiri uhifadhi endelevu. Kwa siku nzima ya leo, anga la Tabora ...

MAAFISA MAENDELEO IBUENI FURSA KWA JAMII - FELISTER MDEMU

Naibu Katibu Mkuu wa Maendeleo ya Jamii Felister Mdemu ametoa amewahimiza maafisa Maendeleo ya Jamii nchini kuubua fursa za maendeleo katika jamii zao na kuwajengea uwezo wananchi kuhusu namna ya kunufaika na fura hizo. Mdemu amebainisha hayo Oktoba 17,2025 Mkoani Iringa alipotembelea na kukagua uendeshaji wa miradi katika Chuo cha Maendeleo ya Jamii Rungemba. Felister amesema wataalam wa Maendeleo ya Jamii wanatakiwa kwenda mbali zaidi ya kutoa hamasa peke yake kwa wananchi bali wanatakiwa kuhakikisha wanawejengea uwezo wa kuweza kunufaika kupitia fursa wanazoibainisha “Wataalam kutoka Chuo cha Maendeleo ya Jamii Rugemba wamewahamasisha wananchi kushiriki katika kilimo cha parachichi pamoja na kuwalea katika kila hatua ili waweze kunufaika na juhudi zao na kujipatia maendeleo”amesema Felister Vilevile Felister amewapongeza wataalam wa Maendeleo ya Jamii kutoka chuo hicho kwa kutatua changamoto ya lishe katika Mkoa iringa kupitia ubunifu . “Pamoja na Mkoa huu kulima mazao mengi lakini ...

WAANGALIZI WA UCHAGUZI WATAKIWA KUTOINGILIA MCHAKATO WA UCHAGUZI MKUU

Image
  Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe.Jaji wa Mahakama Kuu Asina Omari akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao kazi cha siku moja baina ya Tume na Waangalizi wa Ndani ya Nchi na Wakimataifa wa uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 jijini Dodoma leo Oktoba 17, 2025. Kikao hicho kililenga kuwapa waangalizi hao taarifa za maandalizi ya Uchaguzi pamoja na mambo ya kuzingatia ya kiusalama na afya wakati wa uchaguzi. (Picha na INEC). Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe.Jaji wa Mahakama Kuu Asina Omari akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao kazi cha siku moja baina ya Tume na Waangalizi wa Ndani ya Nchi na Wakimataifa wa uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 jijini Dodoma leo Oktoba 17, 2025. Kikao hicho kililenga kuwapa waangalizi hao taarifa za maandalizi ya Uchaguzi pamoja na mambo ya kuzingatia ya kiusalama na afya wakati wa uchaguzi. (Picha na INEC). Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Kishereia wa INEC , Ndg. Cyprian Mbugano akiwasilisha mada kuhusu maandalizi ya uchaguzi...

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO

Image

SERIKALI YAENDELEA KUIMARISHA HUDUMA ZA USTAWI KWA WAZEE

Image
Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kudumisha huduma bora kwa wazee kwa kuhakikisha kundi hilo linapata huduma za msingi zinazowawezesha kuishi maisha yenye heshima na kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya taifa. Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt. John Jingu tarehe 15, 2025 wakati wa ziara yake katika Makazi ya Wazee Wasiojiweza cha Tushikamane Pamoja Foundation yaliyopo Kata ya Kwembe, Manispaa ya Ubungo mkoani Dar Es Salaam. Dkt. Jingu amesema wazee ni sehemu ya taifa kwakua wamelitumikia kwa muda mrefu kwa uaminifu na kujitolea hivyo jamii ya Watanzania wana wanawajibu wa kuwasaidia na kuwaenzi wazee kama ishara ya kuthamini mchango wao kwa maendeleo ya nchi. “Lengo la kuwatembelea ni kuwaona kuwajulia hali na kuendelea kuwaenzi pamoja na kuthamini mchango wenu mkubwa katika kujenga na kuimarisha jamii yetu ya Tanzania, ninata...

TASACO YAFANIKIWA KUWAWEZESHA WATOTO WENYE UHITAJI KWA KUWAPA MAHITAJI MAALUM

Image
  Taasisi isiyo ya kiserikali ya Tanzania Samaritan Community Organization (TASACO) Imefanikiwa kuwawezesha Jumla ya watoto 50 wenye uhitaji kupata Elimu bora kwa kuwapatia vifaa vya shule na fedha, 48 ni wanafunzi wa shule ya Msingi na Wawili wanasoma shule ya upili. Amezungumza hayo Oktoba 14,2025 Kwenye Mkutano Mkuu wa TASACO uliofanyika kwenye Viwanja vya Mako Makuu ya Taasisi hiyo iliyopo Ilala Jijini Dar es salaam ,Mkurugenzi Paul Chegere amesema kuwa Mradi wao wa Somesha Mtoto mmoja ni kuwasomesha watoto hao ili kuwawezesha kutimiza ndoto zao za kufanikiwa. Chegere amesema kuwa moja ya faida ya Mradi huo ni kutengeneza kizazi chenye utu na kitakachoweza kusaidia kuondoa umasikini na kuletwa Maendeleo yenye tija kwa Taifa. Mkutano Mkuu huo umefanyika ili kufanya tathmini ya Miradi ambayo imefanyika kwa mwaka uliopita,Mkurugenzi Chegere Ameitaja Miradi Miwili itayokwenda kufanyika kwa mwaka 2025 /2026 ambayo ni Bemefo utakaojumuisha Malezi,Afya ya Akili na Elimu bora,Huku Mrad...

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO

Image