Skip to main content

JAJI MWAMBEGELE AKAGUA MWENENDO UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA KWENYE MAGEREZA



Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele leo Juni 28, 2025 ametembelea na kukagua mwenendo wa zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura katika Magereza ya Bukoba, Muleba, Biharamulo mkoani Kagera na Chato mkoani Geita. 

Mzunguko wa tatu wa awamu ya pili ya uboreshaji Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa Wafungwa chini ya miezi sita na mahabusu waliopo katika Magereza kwa Tanzania Bara na Vyuo vya Mafunzo Zanzibar umeanza leo Juni 28, 2025 na utaendelea kwa siku saba hadi Julai 04, 2025

Comments

Popular posts from this blog

SEKTA YA NISHATI IWE KICHOCHEO CHA KUIUNGANISHA AFRIKA KUJENGA UCHUMI