TUME YATANGAZA RATIBA YA VYAMA KUCHUKUA FOMU ZA WAGOMBEA WA URAIS
- Get link
- X
- Other Apps
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Ramadhani Kailima akizungumza wakati akitangaza ratiba na orodha ya vyama ambavyo wagombea wake wa Kiti cha Rais na Makamu wa Rais kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania watafika katika Ofisi za Tume Njedengwa Jijini Dodoma kuchukua fomu za utezi kwaajili ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025. Kailima amesema hadi kufikia leo Agosti 08, 2025 vyama 14 vimeijulisha Tume ratiba ya wagombea wa vyama husika kuchukua fomu. Zoezi hilo litaanza Agosti 09 hadi 27 mwaka huu na vyama vingine vitakavyojitokeza vitapangiwa ratiba.
Na Mwandishi Wetu
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imetangaza ratiba ya kuchukua fomu za uteuzi kwa wagombea wa vyama 14 vya siasa waliopendekezwa kugombea nafasi za Kiti cha Rais na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo inaanza kesho tarehe 09 Agosti, 2025.
“Aidha, ni muhimu tukumbuke kuwa, ratiba hii inahusu vyama kumi na nne (14) pekee vilivyowasilisha taarifa hadi kufikia leo tarehe 08 Agosti, 2025, hivyo iwapo vyama vingine vitajitokeza, tutaandaa ratiba husika na kuwajulisha,” amesema.
Amevipongeza vyama vyote vya siasa kwa kuendelea kufanya maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 na kuongeza kuwa, Tume kwa upande wake itazingatia katiba, sheria na kanuni wakati wote wa mchakato wa uchaguzi.
- Get link
- X
- Other Apps
Comments
Post a Comment