RAIS TUCTA AUPONGEZA UONGOZI JOWUTA KWA KUENDELEA KUUNGANISHA WANACHAMA WAKE

 


Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhokya ameupongeza uongozi wa Chama cha Wafanyakazi Wanahabari Tanzania (JOWUTA) kwa namna ambavyo unajitahidi kuwaleta pamoja Wanahabari na wanachama wake.

Nyamhokya ameitoa kauli hiyo wakati akifungua mafunzo kuhusu fidia kwa wafanyakazi (WCF)kwa wanachama wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanaofanya Kazi katika Vyombo vya Habari (JOWUTA), yaliyofanyika jijini Dar es Salaam Mei 25, 2026.


Amesema suala la kuwajengea uwezo wanachama ni moja ya nyenzo muhimu kwa uhai wa chama chochote cha wafanyakazi na ni muhimu Wafanyakazi  wawe na uelewa wa kutosha kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu maisha yao ya kila siku na jamii inayowazunguka.


Amewataka Wanachama wa JOWUTA kuwa na Umoja na  Mshikamano kwani ndio nguzo kuu na uimara wa Chama chochote chenye malengo ya kunufaika.

Mafunzo hayo yameandaliwa kwa ushirikiano na WCF kwa lengo la kuongeza uelewa kwa wanahabari kuhusu haki, mafao na taratibu za fidia kwa wafanyakazi ili waweze kuripoti masuala hayo kwa usahihi kwa umma.

 
Habari Picha 12230

Ameeleza kuwa WCF ni taasisi ya hifadhi ya jamii iliyoanzishwa kwa mujibu wa sheria kwa ajili ya kuwahudumia wafanyakazi wa sekta ya umma na binafsi wanaopata ajali, kuugua au kufariki kutokana na kazi zao.
Habari Picha 12231
Aidha, amesema mfuko huo unatoa mafao mbalimbali ikiwemo huduma za matibabu, fidia ya ulemavu wa muda na kudumu, msaada kwa wategemezi wa marehemu pamoja na huduma za utengemao.

Nyamhokya amewataka wanahabari kutumia taaluma yao kuwahamasisha waajiri kujisajili WCF na kuwasilisha michango kwa wakati, huku pia wakielimisha wafanyakazi umuhimu wa kujiunga na vyama vya wafanyakazi ili kuimarisha mshikamano katika kutetea haki na maslahi yao.

Comments

Popular posts from this blog

SEKTA YA NISHATI IWE KICHOCHEO CHA KUIUNGANISHA AFRIKA KUJENGA UCHUMI