MAKAMU WA RAIS AFANYA MAZUNGUMZO NA MABALOZI
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Mpango amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi Mhe. Suzan Kaganda anayekwenda kuiwakilisha Tanzania nchini Zimbabwe pamoja na Balozi Mhe. Dkt. Habib Kambanga anayekwenda kuiwakilisha Tanzania nchini Rwanda. Mazungumzo hayo yamefanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam leo tarehe 28 Machi 2025. Katika mazungumzo hayo Makamu wa Rais amewapongeza Mabalozi hao kwa kuteuliwa na imani waliopewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuliwakilisha Taifa kwenye nchi hizo. Aidha amewasihi kulinda na kutetea maslahi ya Taifa. Makamu wa Rais amewasisitiza Mabalozi hao kuwa na takwimu za msingi kuhusu maendeleo ya kijamii na kiuchumi ya Tanzania ili kuwa na uwakilishi mzuri katika maeneo yao hususani katika kutekeleza diplomasia ya uchumi. Pia amewataka kufanya jitihada za makusudi kuzifahamu vema nchi wanazokwenda kuiwakilisha Tanzania ili kuweza kujifunza misingi ya ukuzaji wa uchumi wao na kuhamish...