Posts

AMANI NI JUKUMU LETU TUSHIRIKIANE NA VYOMBO VYA USALAMA KUOKOA JAMII

Image
Jeshi la Polisi Tanzania limethibitisha kuwa hali ya usalama nchini imeendelea kuwa shwari. Hata hivyo, ukweli ni kwamba amani ya nchi yetu inategemea zaidi uelewa wa kila Mtanzania kuhusu umuhimu wa kulinda na kuimarisha utulivu mahali alipo. Amani ndiyo nyenzo kuu na ya msingi inayotuwezesha sote kushiriki na kufanya shughuli halali zinazotupatia mahitaji yetu ya kila siku bila hofu. Ili Jeshi la Polisi liweze kutekeleza majukumu yake kikamilifu ya kulinda raia na mali zao, ni lazima kuwepo na ushirikiano wa karibu kati ya polisi na wananchi. Raia wema hawapaswi kuwaogopa au kuwakimbia askari, kwani mara nyingi wanaofanya hivyo ni wale wanaojihusisha na vitendo vya uhalifu vinavyoumiza jamii. Kutoa ushirikiano kwa vyombo vya ulinzi ni hatua ya kizalendo inayosaidia kudhibiti uhalifu katika mitaa yetu. Hata hivyo, ili kujenga imani hii, ni muhimu kwa askari wetu kuzingatia weledi kwa kutodhulumu watu kwa jeuri wala kuwashtaki raia kwa uongo. Vilevile, jamii inapaswa kuacha dhana ya ku...

TMA YASISITIZA UMUHIMU WA KUFUATILIA NA KUZINGATIA TAARIFA ZA HALI YA HEWA

Image
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania ( TMA) na Makamu Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Sayansi ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa Duniani ( IPCC) Dkt. Ladislaus Chang'a akieleza umuhimu wa kufuatilia na kuzingatia taarifa za hali ya hewa pamoja na tahadhari za hali mbaya ya hewa wakati wa kikao cha cha kamati ya Wataalam ya Kitaifa ya Usimamizi wa Maafa tarehe 19 Disemba, 2025 Jijini Dodoma Kikao hicho kiliongozwa na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Dkt. Jim Yonazi.

WAZIRI MBARAWA ARIDHISHWA NA MAENDELEO YA UJENZI WA BANDARI MPYA YA KISIWA MGAO MTWARA ILIYOFIKIA ASILIMIA 25.

Image
  Waziri wa Uchukuzi, Mhe. Prof. Makame Mbarawa, ameridhishwa na maendeleo ya mradi wa Usanifu na Ujenzi wa Bandari Mpya ya Kisiwa Mgao, mkoani Mtwara, ambao umefikia asilimia 25 ya utekelezaji wake.  Akizungumza baada ya ziara yake ya kutembelea na kukagua mradi huo,tarehe 20 Disemba,2025, Waziri  Prof. Mbarawa ameeleza kuridhishwa na kasi ya utekelezaji pamoja na ubora wa kazi zinazoendelea kufanyika katika eneo la mradi. Waziri Prof. Mbarawa amesema Bandari mpya ya Kisiwa Mgao ni mradi wa kimkakati unaolenga kuimarisha sekta ya uchukuzi wa majini na kukuza uchumi wa Taifa, hususan kwa ukanda wa Kusini, hivyo ni wajibu wa TPA na wadau wote kuhakikisha mradi unatekelezwa kwa kuzingatia ubora, uwazi na matumizi sahihi ya rasilimali za umma. Aidha, Waziri Mbarawa alibainisha kuwa kukamilika kwa Bandari ya Kisiwa Mgao kutaongeza uwezo wa nchi katika kuhudumia shehena ya mzigo mchafu, kupunguza msongamano wa shughuli za bandari ya Mtwara, na kuimarisha biashara pamoja na usa...

WAZIRI MKUU AKAGUA MRADI UNAOJENGWA KWA USHIRIKIANO NA MRADI WA LNG NA TPDC, LINDI

Image
Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba leo Desemba 20, 2025 amekagua maendeleo ya mradi wa shule mpya ya msingi ya Likong’o inayojengwa kwa ushirikiano na Mradi wa LNG na TPDC. Shule hiyo iliyopo katika kijiji cha Likong’o itagharimu kiasi cha shilingi bilioni 1.2 pale itakapokamilika, ambapo kati ya fedha hizo, Serikali imechangia asilimia 26.6, kampuni ya Shell imechangia asilimia 36.6 na kampuni ya Equinor imechangia asilimia 36.6. Akizungumza na wakazi wa eneo hilo, Dkt. Mwigulu ametoa wito kwa wakazi wa eneo hilo na  Tanzania kwa ujumla kuwapeleka watoto wao shuleni kwani Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameweka mazingira wezeshe katika sekta ya elimu yanayowafanya watoto wa kitanzania kupata elimu bora. “Rais Dkt. Samia aliahidi ajira za walimu katika siku 100, sasa usaili umefanyika na walimu 7000 wataajiriwa na itakapofika Januari 10, 2026 walimu hawa wataripoti katika vituo vya kazi watakavyopangiwa” Naye, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI Reuben Kwagilwa amesema kuwa Rais...

KIKAO CHA KAMATI YA WATAALAM YA KITAIFA YA USIMAMIZI WA MAAFA CHAPITISHA MIONGOZO YA KUKABILIANA NA MAAFA NCHINI

Image
  Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Dkt. Jim Yonazi ameongoza Kikao cha Kamati ya Wataalam ya Kitaifa ya Usimamizi wa Maafa leo 19 Desemba,2025 kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano uliopo Ofisi ya Waziri Mkuu Ngome, Jijini Dodoma. Katika kikao hicho, Mpango wa Taifa wa dharura wa  kukabiliana na Ukame, Mafuriko na Majanga mengine yanayohusiana kwa kipindi cha Novemba 2025 hadi Juni 2026 umejadiliwa na kupokelewa na wajumbe wa kikao. Aidha, Miongozo ya uanzishwaji na Uendeshaji wa kituo cha operesheni na Mawasiliano ya dharura na Timu ya kukabiliana na Dharura ngazi ya Taifa na Mkoa imejadiliwa na kupitishwa na wajumbe wa kikao. Miongozo iliyojadiliwa na kupitishwa ni pamoja na, Mwongozo wa Uanzishaji wa kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura, Mwongozo wa Uendeshaji wa kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura Ngazi za Mikoa, Mwongozo wa Uanzishaji na Uendeshaji wa Timu ya Mkoa ya kukabiliana na Dharura. Pia, Muongozo wa Ua...

GRAPHITE YAANZA KUZALISHWA MOROGORO

Image
MOROGORO Naibu Waziri wa Madini, Mhe. Dkt. Steven Kiruswa, amezitaka kampuni zinazojishughulisha na shughuli za madini nchini kuhakikisha zinazingatia kikamilifu utunzaji wa mazingira katika maeneo yote ya utekelezaji wa miradi yao. Dkt. Kiruswa ameyasema hayo leo, Desemba 19, 2025, baada ya kutembelea mradi wa uchimbaji na uchenjuaji wa madini mkakati ya kinywe (graphite) unaotekelezwa na Kampuni ya Synergy Tanzania Company Ltd (STCL) katika kijiji cha Kisanzala, Kata ya Lundi, Wilaya ya Morogoro, mkoani Morogoro. Akizungumza katika ziara hiyo, Dkt. Kiruswa ameipongeza kampuni hiyo kwa kufikia hatua ya kuanza uzalishaji wa madini mkakati kwa matumizi ya teknolojia ya kisasa duniani, huku akisisitiza umuhimu wa utunzaji wa mazingira sambamba na maendeleo ya kiuchumi. “Nachukua fursa hii kuwapongeza kwa hatua mliyofikia ya kuanza uzalishaji wa madini haya muhimu katika teknolojia ya kisasa. Hata hivyo, ni muhimu kuhakikisha mnatunza mazingira ipasavyo na kuwasilisha mpango wa ulinzi wa ...

INGIENI KATIKA DUNIA YA KAZI KWA MOYO WA UADILIFU-DKT AKWILAPO

Image
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo amewataka wahitimu wa chuo cha ardhi Tabora (ARITA) kuingia kwenye dunia ya kazi kwa moyo wa uadilifu, uzalendo na ubunifu.  Amesema, Taifa linawategemea wahitimu hao sambamba na kuhitaji wataalamu wanaoweza kutumia elimu kwa manufaa ya wote na si kwa maslahi binafsi. "Tumieni utaalamu wenu kwa weledi, uadilifu na kufuata sheria. Epukeni kabisa mambo ya rushwa na ufisadi". Amesema. Mhe. Dkt Akwilapo ametoa kauli hiyo leo tarehe 19 Desemba 2025 katika Mahafali ya 43 Chuo cha Ardhi Tabora (ARITA) yaliyofanyika chuoni hapo mkoani Tabora. Aidha, amewataka wahitimu hao wa chuo cha ARITA kuendelea kujifunza kwa kuwa  elimu haina mwisho na kusisitiza kuwa anataka kuona elimu waliyoipata inakuwa  na manufaa kwa Taifa na sio machungu kwa Taifa. "Muwe mabalozi wema wa Chuo. Msidanganyike na yanayoandikwa kwenye mitandao kwamba nyie ni kundi la wanajamii wenye ukaidi, wasio na utii, wala heshima kwa wazazi, vio...