UDART,DART ZATAKIWA KUSHIRIKIANA KUTATUA KERO USAFIRI WA MWENDOKASI
Mchengerwa ametoa maagizo hayo leo jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa Mageti Janja na Kadi Janja ambazo zitatumika kufanya malipo ya nauli katika usafiri wa mabasi yaendayo haraka hali itakayosaidia kujibu maswali ya watanzania kuhusu changamoto za usafiri wa mwendo kasi.
Awali akizungumzia uzinduzi wa Mageti janja na Kadi Janja, amesema pongezi ziende kwa Dart kutokana na kuja na mfumo huo ambao unakwenda kujibu maswali ya namna ya ukusaji nauli kwa kuachana na karatasi na kuanzia kesho kadi zitaanza kutumika ni mapinduzi makubwa katika huduma uya usafiri.
Ameongeza kuwamfumo huo wa kutumia kadi unafanya usafiri wa mwendokasi kuwa katika kiwango cha juu, “ hivyo niwapongeze Dart kwa kutekeleza agizo la Kamati ya Bunge na dhamira ya Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kujibu hoja kwa wananchi katika changamoto zilizokuwa zikiwabili katika ulipaji wa nauli.
Pia amesisitiza kwa Dart kuhakikisha wanawachukulia hatua kali madereva wanaokwenda kinyume na sheria na taratibu ikiwemo kuacha abiria katika vituo, ilihali mabasi yao yakiwatupu na wale wenye lugha chafu kwa abiria.

Comments
Post a Comment